Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 4:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Huyo mutu alipotaja tu Sanduku la Mungu, Eli alianguka machali kutoka kwenye kiti chake pembeni ya mulango. Eli alipoanguka hivyo, shingo yake ilivunjika maana alikuwa muzee na munene, naye akakufa. Eli alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka makumi ine.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 4:18
15 Referans Kwoze  

Nimekuwa mugeni kwa wandugu zangu, kaka na dada zangu hawanitambui.


Ninamwambia Mungu, yeye kikingio changu: “Kwa nini umenisahau? Kwa nini niende huko na huko nikiomboleza kwa kuteswa na adui yangu?”


Ninasikia kiu ya Mungu, kiu ya Mungu Mwenye Uzima. Nitafika kwake wakati gani na kuuona uso wake?


Ee Yawe, ninapenda makao yako, pahali utukufu wako unapokaa.


Eli, akiwa na wasiwasi ndani ya moyo juu ya Sanduku la Mungu, alikuwa ameikaa kwenye kiti chake, pembeni ya barabara akiangalia. Yule mutu alipofika katika muji na kueleza habari hizo, muji muzima ulilia kwa sauti.


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Yule aliyeleta habari akasema: “Waisraeli wamewakimbia Wafilistini. Kumekuwa mauaji makubwa kati ya Waisraeli. Zaidi ya yote, wana wako wote wawili, Hofuni na Finehasi, wameuawa, na Sanduku la Agano la Mungu limetekwa.”


Tena ilitokea kwamba, mukwe wa Eli, ni kusema muke wa Finehasi, kwa wakati ule alikuwa na mimba, na muda wake wa kuzaa ulikuwa umekaribia. Aliposikia kwamba Sanduku la Agano la Mungu limetekwa na kwamba baba mukwe wake, hata na mume wake wamekufa, mara moja akapata maumivu ya kuzaa. Kwa hiyo akachutama na kuzaa.


Samusoni akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kwa miaka makumi mbili, nyakati za Wafilistini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite