Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 3:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Samweli aliendelea kukomaa na Yawe akakuwa pamoja naye, na yale yote aliyosema hakuna hata moja ambalo halikutimia.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 3:19
32 Referans Kwoze  

Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


Yule mutumishi akamwambia: “Ngoja kidogo. Katika muji huu kuna mutu wa Mungu ambaye anaheshimiwa sana. Kila neno analosema linakuwa kweli. Sasa tumwendee. Labda anaweza kutuambia jinsi safari yetu itakavyokuwa.”


“Atukuzwe Yawe ambaye amewapatia watu wake Waisraeli amani, kulingana na ahadi yake. Ametimiza ahadi zake zote njema alizozitoa kupitia kwa mutumishi wake Musa.


Na Yesu alizidi kuwa na hekima, na kuongezeka kimo na kuendelea kumupendeza Mungu na watu.


Bwana akulinde. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.


Yawe alimusikilia Hana huruma naye akajaliwa kupata watoto wa kiume watatu na wabinti wawili. Mutoto Samweli akaendelea kukomaa mbele ya Yawe.


Basi kwa kumaliza, wandugu zangu, kwa heri. Mujikaze kuwa wakamilifu, mufarijiane ninyi kwa ninyi, mukuwe na nia moja, muishi katika amani, na Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.


Mutoto yule akakomaa, akazidi kuwa na nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.


Mutoto yule akakomaa na kuzidi kuwa na nguvu katika roho. Akakaa katika nafasi za jangwa mpaka siku alipojionyesha waziwazi mbele ya Waisraeli.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Wakati ule, Abimeleki pamoja na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akamwendea Abrahamu, akamwambia: “Mungu yuko pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.


Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”


Kisha muke wa Manoa akazaa mutoto mwanaume, naye Manoa akamupa jina la Samusoni. Mutoto huyo akakomaa naye Yawe akamubariki.


Mimi niko pamoja nawe, nitakulinda popote utakapoenda na kukurudisha katika inchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapotimiza ahadi niliyokupa.”


Sasa, munakuwa na mufalme wa kuwaongoza. Kwa upande wangu, mimi ni muzee mwenye imvi, na wana wangu wako pamoja nanyi. Nimekuwa kiongozi wenu tangu nilipokuwa kijana mpaka sasa.


Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”


Yule bwana wake akatambua kwamba Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, na kwamba ndiye aliyefanikisha mambo yote Yosefu aliyofanya.


Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.


Hakuna hata ahadi yoyote njema ambayo Yawe aliiahidi Waisraeli ambayo haikutimia. Ahadi zote zilitimia.


Mutoto Samweli aliendelea kukomaa, akazidi kupendwa na Yawe na watu.


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Kokote Daudi alikotumwa na Saulo, Daudi alifanikiwa. Hivyo, Saulo akamufanya kuwa mukubwa wa waaskari wake. Jambo hilo liliwafurahisha watu wote hata watumishi wa Saulo.


Saulo alikuwa anamwogopa Daudi kwa sababu Yawe alikuwa pamoja naye, lakini Yawe alikuwa amemwacha Saulo.


Mujue kwamba maneno yote Yawe aliyosema juu ya jamaa ya Ahabu yametimia. Yawe ameyafanya hayo aliyosema kwa njia ya mutumishi wake Elia.”


Basi tukio hilo lilitokana na ahadi ya Yawe kwa mufalme Yehu, kusema: “Wazao wako watatawala Israeli mpaka kizazi cha ine.”


Yawe anasema hivi: Nitaleta uovu juu ya pahali hapa na juu ya wakaaji wake kama vile inavyokuwa katika kitabu kilichosomwa na mufalme wa Yuda.


ni vilevile na neno langu mimi: halitanirudilia bila mafanikio, lakini litatimiza mapenzi yangu, litafikia shabaha nililoliwekea.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite