Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 3:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Basi, Samweli akamwelezea Eli yote aliyoambiwa, bila kumuficha chochote. Halafu Eli akasema: “Yeye ni Yawe; afanye anachoona ni chema kwake.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 3:18
18 Referans Kwoze  

Naye Hezekia akamwambia Isaya: Neno la Yawe ulilosema ni zuri. Alisema hivyo maana alifikiri: Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.


Akamujibu: “Wewe unasema kama wanawake wapumbafu. Tukipokea mazuri kutoka kwa Mungu, kwa nini tukatae kupokea vilevile mabaya kutoka kwake?” Katika mambo hayo yote, Yobu hakusema neno lolote la kumukosea Mungu.


Basi mujinyenyekeze mbele ya Mungu mwenye uwezo, kusudi awainue kwa wakati unaofaa.


Lakini Waisraeli wakamwambia Yawe: “Tumetenda zambi. Utufanye vile unavyopenda, lakini tunakuomba utuokoe leo.”


Kwa nini mutu anungunike ikiwa ameazibiwa kwa ajili ya zambi zake?


Uniokoe katika makosa yangu yote; usikubali wapumbafu wanichekelee.


akisema: Nilikuja uchi katika dunia, nitaondoka uchi katika dunia. Yawe amenipa, Yawe ametwaa. Jina la Yawe litukuzwe.


Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Yawe akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Musa, akataja jina lake: Yawe.


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Lakini ujipe moyo! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu. Naye Yawe atutendee lile analoona ni jema kwake.”


Lakini ikiwa Yawe hapendezwi nami basi, mimi niko tayari; na anitendee sawa vile anavyotaka.”


Naye Hezekia akamwambia Isaya: “Neno la Yawe ulilosema ni zuri.” Alisema hivyo maana alifikiri: “Kutakuwa amani na salama muda wote wa maisha yangu.”


Kisha, nabii Yeremia akamwelezea Zedekia, mufalme wa Yuda, maneno hayo yote huko Yerusalema,


Wakati fulani mufalme Zedekia alitaka kumwona nabii Yeremia. Basi, akaagiza Yeremia aletwe kwenye mulango wa tatu wa nyumba ya Yawe. Huko, mufalme alimwambia Yeremia: Ninataka kukuuliza jambo fulani; usinifiche kitu chochote.


Yeremia akawajibu: Vema; nimesikia. Nitamwomba Yawe, Mungu wenu, kama mulivyonisihi; jibu lolote Yawe atakalonipa, nitawaambia; sitawaficha kitu chochote.


Basi ukuwe hodari! Tupigane kama wanaume kwa ajili ya watu wetu, na kwa ajili ya miji ya Mungu wetu; na Yawe atutendee sawa na mapenzi yake.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite