Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 3:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kisha, Yawe akamwambia Samweli: “Ninataka kutenda jambo fulani katika Israeli ambalo kila mutu atakayesikia, atashituka kwa kulisikia.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 3:11
11 Referans Kwoze  

Mungu akasema: Muangalie mataifa, muone! Mustaajabu na kushangaa. Maana ninatenda kitu ukiwa bado unaishi, kitu ambacho ungeambiwa haungesadiki.


‘Muangalie, ninyi wenye kuzarau, mupigwe na mushangao na mutoweke! Maana katika siku hizi nitafanya jambo ambalo ninyi musingeweza kusadikia hata wangewaelezea.’ ”


Utasema hivi: Musikilize neno la Yawe, enyi wafalme wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalema. Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kweli ninaleta hasara kwenye nafasi hii, hata kila mumoja atakayesikia habari ile, atastajabu.


basi, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nitaleta juu ya Yerusalema na Yuda hasara ambayo hata yeyote atakayesikia atashituka.


Watu watazimia kwa ajili ya hofu, wakingojea mambo yatakayotokea katika dunia, kwa maana vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu, mambo ya ajabu na ya kushangaza. Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima, na akili ya wenye akili wao itatoweka.


Kila mara itakapopita kwenu itawapata; nayo itapita kila asubui, muchana na usiku. Kusikia ujumbe huu tu kutakuwa kitisho.


Kisha Yawe akakuja na kusimama hapo, akamwita Samweli kama pale mbele: “Samweli! Samweli!” Samweli akasema: “Sema, maana mimi mutumishi wako ninasikiliza.”


Wafilistini walipiga vita, na Waisraeli walishindwa na kukimbia kila mutu kwake. Siku hiyo kulikuwa mauaji makubwa maana waaskari wa miguu elfu makumi tatu wa Israeli waliuawa.


Imeunganishwa pamoja, hata haiwezekani kuitenganisha.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite