‘Muangalie, ninyi wenye kuzarau, mupigwe na mushangao na mutoweke! Maana katika siku hizi nitafanya jambo ambalo ninyi musingeweza kusadikia hata wangewaelezea.’ ”
Utasema hivi: Musikilize neno la Yawe, enyi wafalme wa Yuda nanyi wakaaji wa Yerusalema. Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kweli ninaleta hasara kwenye nafasi hii, hata kila mumoja atakayesikia habari ile, atastajabu.
Hivyo, nitawatendea tena watu hawa maajabu, mambo ya ajabu na ya kushangaza. Nao wenye hekima wao wataishiwa hekima, na akili ya wenye akili wao itatoweka.
Wafilistini walipiga vita, na Waisraeli walishindwa na kukimbia kila mutu kwake. Siku hiyo kulikuwa mauaji makubwa maana waaskari wa miguu elfu makumi tatu wa Israeli waliuawa.