5 Saulo alipoona kundi la waaskari wa Wafilistini, alianza kuogopa, akaanza kutetemeka kwa hofu aliyokuwa nayo ndani ya moyo wake.
Basi, mufalme akabadilika rangi na kufazaika kwa ajili ya mawazo yaliyomufikia, viungo vyake vikaregea na magoti yakaanza kutetemeka.
Mufalme wa Yuda alipopata habari kwamba Waaramu wanashirikiana na Waisraeli, yeye pamoja na watu wote wa Yuda waliogopa na kutetemeka kama miti inayotikiswa na upepo.
Kitu mutu mwovu anachoogopa ndicho kitakachomupata, lakini kitu mwenye haki anachotamani ndicho atakachopewa.
Wanaangamizwa kwa rafla, wateketezwe kabisa kwa vitisho.
Hofu kubwa inamutisha kila upande, inamufuata katika kila hatua yake.
Sauti za vitisho zitamupigia kelele katika masikio. Anapozani amestawi, mwangamizi atamushambulia.
Wafilistini walikusanyika na kupiga kambi yao kule Sunemi; na Saulo aliwakusanya Waisraeli wote na kupiga kambi yao kwenye mulima Gilboa.
Hata alipomwomba Yawe shauri, Yawe hakumujibu kwa ndoto, kwa mawe ya kupiga kura, wala kwa njia ya manabii.