Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 26:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kwa hiyo usiku, Daudi na Abisai wakaingia kwenye kambi ya Saulo, wakamukuta Saulo amelala katikati ya kambi hiyo, na mukuki wake umechomekwa katika udongo karibu na kichwa chake. Abeneri pamoja na waaskari walikuwa wamelala na kumuzunguka Saulo.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 26:7
5 Referans Kwoze  

Uwaambie vilevile wapeleke kutoka hapa magari ya kukokotwa ya kuwaleta watoto wao wachanga na wake zao. Wala wasikose kumuleta baba yao.


Kesho yake, Daudi aliamuka asubui mapema, na akamwachia muchungaji mumoja kondoo. Alibeba chakula na kwenda kama vile alivyoagizwa na baba yake Yese. Alipofika kwenye kambi ya Waisraeli, aliwakuta wanajipanga kwenye sehemu yao ya vita na wanapiga kelele za vita.


Daudi akamwambia Ahimeleki ambaye alikuwa Muhiti, na Abisai ndugu ya Yoabu (mama yao aliitwa Zeruya): “Nani atakwenda pamoja nami kwenye kambi ya Saulo?” Abisai akamwambia: “Mimi nitakwenda pamoja nawe.”


Abisai akamwambia Daudi: “Leo Mungu amemutia adui yako katika mikono yako. Basi, uniache nimushindilie katika udongo kwa pigo moja tu la mukuki. Sitamupiga mara mbili.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite