Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 26:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Daudi akatoka, akaenda pahali Saulo alipopiga kambi. Akaona pahali ambapo Saulo alikuwa amelala. Saulo alikuwa pamoja na Abeneri mwana wa Neri, mukubwa wa waaskari, katikati ya kambi akizungukwa na waaskari wake.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 26:5
10 Referans Kwoze  

Saulo alipomwona Daudi akienda kupigana na yule Mufilistini Goliati, alimwuliza Abeneri, jemadari wa kundi lake: “Abeneri, huyu ni kijana wa nani?” Abeneri alijibu: “Ee Mufalme, ninaapa kwa jina lako, mimi sijui.”


Kesho yake, Daudi aliamuka asubui mapema, na akamwachia muchungaji mumoja kondoo. Alibeba chakula na kwenda kama vile alivyoagizwa na baba yake Yese. Alipofika kwenye kambi ya Waisraeli, aliwakuta wanajipanga kwenye sehemu yao ya vita na wanapiga kelele za vita.


Neri alizaa Kisi, naye Kisi alizaa Saulo. Saulo alikuwa na wana wane: Yonatani, Malikisua, Abinadabu na Esibali.


Abeneri aliporudi Hebroni, Yoabu alimupeleka pembeni kwenye mulango sawa vile anataka kuzungumuza naye kwa siri. Hapo Yoabu akamukata Abeneri katika tumbo kwa sababu Abeneri alikuwa amemwua ndugu yake Asaeli, na Abeneri akakufa.


Katika kabila la Benjamina, kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyeitwa Kisi. Yeye alikuwa mwana wa Abieli, mujukuu wa Zerori, wa jamaa ya Bekorati mwana wa Afia wa kabila la Benjamina.


alituma wapelelezi, akafahamishwa kwamba ni kweli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite