Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 26:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 26:19
32 Referans Kwoze  

Mimi ni mumoja wa wale wanaopenda amani na uaminifu katika Israeli. Sasa wewe unakusudia kuuharibu muji ambao ni sawa vile katika Israeli. Kwa nini sasa unataka kuuangamiza muji unaokuwa mali ya Yawe?”


Tena mufalme Daudi akamwambia Abisayi na hata watumishi wake wote: “Ikiwa mutoto wangu mwenyewe anayawinda maisha yangu, si ni zaidi kwa mutu wa kabila la Benjamina? Ninyi muache anilaani maana Yawe amemwagiza anilaani.


Maana mufalme atanisikiliza na kuniokoa toka katika mikono ya mutu ambaye anataka kuniangamiza mimi pamoja na mwana wangu kutoka urizi wa Mungu.


Ole wangu maana ninaishi kama mugeni huko Meseki; ninaishi kama mugeni katika mahema ya Kedari.


Shetani akaenda kinyume cha Waisraeli, akamushawishi Daudi kuwahesabu watu.


Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Alesanduro, yule mufua vyuma amenitendea mabaya mengi. Bwana atamulipa kufuatana na matendo yake.


Heri wale wanaoleta fujo kati yenu wangejikata viungo vyao vya uzazi.


Kama ukimuhuzunisha ndugu yako kwa sababu ya chakula unachokula, wewe hautendi tena kufuatana na upendo. Kwa njia ya chakula chako usimupoteze mutu ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.


Halafu utaona na utafurahi, moyo wako utasisimuka na kushangilia. Maana utajiri tokea ngambo ya bahari utakufikia kwa wingi, mali za mataifa zitaletwa kwako.


Usimuchongee mutumwa kwa bwana wake, kusudi asikulaani, na kuonekana kwamba uko na kosa.


Yawe akamwuliza: ‘Kwa namna gani?’ Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; basi, kwenda ufanye hivyo.’


Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda.


Alijitupa kwenye miguu ya Daudi na kumwambia: “Bwana wangu, kosa lote likuwe juu yangu tu. Ninakuomba niongee nawe mimi mujakazi wako. Ninakuomba usikilize maneno ya mujakazi wako.


Miji yenu nitaiteketeza, pahali penu patakatifu nitapafanya jangwa na harufu zenu nzuri za sadaka sitazikubali.


Halafu Yuda akamukaribia Yosefu na kumwambia: “Bwana, ninakuomba uniruhusu mimi mutumishi wako, nijitetee mbele yako kwa maneno machache. Ninakusihi usinikasirikie, maana wewe ni kama mufalme wa Misri mwenyewe.


Kisha, Daudi naye akasimama, akatoka ndani ya pango na kumwita Saulo: “Bwana wangu mufalme!” Mufalme Saulo alipoangalia nyuma, Daudi aliinama mpaka chini, kwa kumuheshimu Saulo.


Daudi akajisemesha ndani ya moyo: “Siku moja, Saulo ataniangamiza. Jambo zuri kwangu ni kukimbilia katika inchi ya Wafilistini. Saulo atakata tamaa kunitafuta ndani ya mipaka ya inchi ya Israeli, nami nitakuwa salama kutoka katika mikono yake.”


Daudi akawauliza Wagibeoni: “Niwatendee nini? Nitalipa namna gani maovu muliyotendewa kusudi mupate kuibariki inchi hii na watu wa Yawe?”


kusudi urizi wa Waisraeli usihamishiwe kwa kabila lingine; kila Mwisraeli atabakia na urizi wa kabila lake.


Hivyo hakutakuwa urizi wowote utakaohamishwa kutoka kabila moja kwa lingine. Kila kabila la Waisraeli litashikilia urizi wake.


kisha neno, vitambulisho au maajabu aliyowaambia yakitokea, na akisema: ‘Tufuate miungu mingine, miungu ambayo hamujapata kuijua, na tuitumikie’,


Lakini mufalme akamwambia: “Kuna maneno gani kati yangu na ninyi wana wa Zeruya? Ikiwa Yawe amemwambia: ‘Umulaani Daudi’, nani sasa anaweza kuuliza: ‘Kwa nini umefanya hivyo?’ ”


Akumbuke sadaka zako zote; akubali sadaka zako za kuteketezwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite