Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 24:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha, Daudi naye akasimama, akatoka ndani ya pango na kumwita Saulo: “Bwana wangu mufalme!” Mufalme Saulo alipoangalia nyuma, Daudi aliinama mpaka chini, kwa kumuheshimu Saulo.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 24:9
19 Referans Kwoze  

Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.


Nao ulimi ni kama moto. Ulimi ni kiungo kinachojaa ubaya wa kila namna. Ulimi unapatikana kwenye nafasi yake katikati ya viungo vyetu, nao ndio unaochafua mwili wote. Unateketeza maisha yetu ukichomwa wenyewe na moto unaotoka katika jehenamu.


Anayesema uongo anachukia wale anaowaumiza, naye anayebembeleza analeta maangamizi.


Upepo wa kaskazini unaleta mvua; vilevile mwenye kusingiziana analeta chuki.


Maneno ya muchongeaji ni kama chakula kitamu ambacho kinashuka mpaka ndani kabisa ya tumbo.


Mutenda maovu anasikiliza maneno mabaya; mwongo anategea sikio ulimi mudanganyifu.


Mutu mupotovu anatawanya ugomvi, na muchonganishi anatenganisha warafiki.


Wakubwa wao watakapopondwa juu ya mawe, ndipo watatambua kwamba maneno yangu yalikuwa mazuri.


Nitateketeza yule anayemuteta mwenzake, sitamuvumilia mwenye majivuno na kiburi.


Basi, sasa bwana wangu mufalme, usikie maneno ya mutumishi wako. Ikiwa Yawe ndiye aliyekuchochea ukuje kunishambulia, basi, apokee sadaka ambayo itamusukuma kubadilisha mawazo yake. Lakini ikiwa ni watu, basi, Yawe awalaani watu hao maana wamenifukuza kutoka urizi ambao Yawe aliotupa wakisema: ‘Kwenda uitumikie miungu mingine.’


Usipitepite hata kidogo ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usitie maisha ya mwenzako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ni Yawe.


Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”


Kwa maneno hayo, Daudi akawashawishi watu wake wasimuzuru Saulo; aliwakataza wasimushambulie. Kisha Saulo akasimama, akatoka ndani ya pango akaendelea na safari yake.


Kisha akamwambia: “Kwa nini unawasikiliza watu wanaokuambia: ‘Daudi anataka kukuzuru’?


Halafu akaendelea kusema: “Lakini kwa nini, wewe bwana wangu unanifuatilia mimi mutumishi wako? Nimefanya nini? Ni uovu gani nimekufanyia?


Halafu Yeremia akamwuliza mufalme Zedekia: Nimekukosea nini, au nimewakosea nini watumishi wako au watu hawa, hata unitie katika kifungo?


Yule kijana alipokwisha kuondoka, Daudi akasimama na kutoka pahali alipojificha karibu na lundo la mawe. Aliinama chini kwa heshima mara tatu mbele ya Yonatani. Wote wawili, Daudi na Yonatani, wakakumbatiana na kulia. Daudi alikuwa na uchungu zaidi kuliko Yonatani.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite