Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 24:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Mutu akimukamata adui yake atamwacha aende salama? Kwa lile ulilonitendea, Yawe akupe zawadi njema!

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 24:20
12 Referans Kwoze  

Yonatani akamwambia: “Usiogope, baba yangu Saulo hatakupata. Wewe utakuwa mufalme wa Israeli, mimi nitakuwa wa pili wako. Hata Saulo baba yangu anajua jambo hili.”


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Wale watu wenye elimu walipokwisha kwenda, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto na kumwambia: “Amuka, utwae mutoto pamoja na mama yake na mukimbilie Misri. Mukae kule mpaka nitakapokuambia kwamba urudie, kwa maana Herode anamutafuta mutoto kusudi amwue.”


kwa sababu amenyoosha mukono wake apigane na Mungu na kujivuna kumupinga yule Mungu Mwenye Uwezo.


Lakini sasa ufalme wako hautadumu kwa sababu amri Yawe aliyokuamuru haukuitii. Yawe amejitafutia mutu mwingine ambaye atamutii kwa moyo wote, na huyo ndiye ambaye atamuchagua kuwa mutawala juu ya watu wake.”


Yawe akubariki kwa yote uliyoyafanya. Yawe wa Israeli uliyemukimbilia akulinde chini ya mabawa yake, akupe zawadi kamilifu.”


Saulo akamwambia Daudi: “Mungu akubariki mwana wangu Daudi. Utafanya mambo makubwa, nawe utafanikiwa katika yote.” Basi, Daudi akaenda zake; Saulo naye akarudi kwake.


kama nimemurudishia rafiki yangu mabaya pahali pa mema, au nimemunyanganya adui yangu bila sababu,


Adui yako akiwa na njaa, umupe chakula; akiwa na kiu, umupe maji ya kunywa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite