Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 22:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Lakini Abiatari, mumoja wa watoto wa kiume wa Ahimeleki mwana wa Ahitubu, aliponyoka akakimbilia kwa Daudi.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 22:20
15 Referans Kwoze  

Abiatari mwana wa Ahimeleki, alipokimbilia kwa Daudi kule Keila, alikwenda na kizibao cha kuhani.


Daudi akamwambia kuhani Abiatari mwana wa Ahimeleki: “Uniletee kizibao cha kuhani.” Abiatari akamupelekea.


Daudi aliposikia mipango miovu ya Saulo juu yake, akamwambia kuhani Abiatari: “Ulete hapa kile kizibao cha kuhani.”


Mara moja upepo mukali ukavuma kutoka katika jangwa, ukaipiga nyumba ile kila upande nayo ikawaangukia, na vijana wote wamekufa. Ni mimi tu peke yangu nimepona kwa kuja kukuletea habari.”


Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.


Mutu wako ambaye sitamwangamiza kutoka mazabahu yangu atakuwa ameponyoka kusudi nipofushe macho yake, naye atakufa moyo na wazao wake watauawa kifo kibaya.


Sewa alikuwa katibu. Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani.


Ahiya mwana wa Ahitubu ndugu yake na Ikabodi mwana wa Finehasi mujukuu wa Eli kuhani wa Yawe katika muji wa Shilo, alikuwa ndiye aliyevaa kizibao cha kuhani. Watu hawakujua kwamba Yonatani amekwisha ondoka.


Abiatari alimwelezea Daudi kwamba Saulo amewaua makuhani wa Yawe.


Kuhani Abiatari akatoka, hata na kuhani Zadoki akatoka pamoja na Walawi wote wakilibeba Sanduku la Agano la Mungu. Wakaliweka lile Sanduku la Mungu chini, mpaka watu wote walipopita kutoka Yerusalema.


Adonia akafanya shauri na Yoabu mwana wa Zeruya, na kuhani Abiatari. Nao wakamufuata na kumwunga mukono.


Daudi akawaita makuhani wawili, Zadoki na Abiatari, na Walawi sita, Urieli, Asaya, Yoeli, Semaya, Elieli na Aminadabu;


Zadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiatari walikuwa makuhani; Sausa alikuwa katibu;


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite