Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 22:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Saulo akawaambia walinzi waliokuwa wakisimama pembeni yake: “Mugeuke na kuwaua makuhani wa Yawe, maana wao wanapatana na Daudi; walijua kwamba ametukimbia wala hawakuniarifu.” Lakini walinzi hao hawakuinua mikono yao kwa kuwaua makuhani wa Yawe.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 22:17
15 Referans Kwoze  

Lakini kwa sababu wazalishaji wale walimwogopa Mungu, hawakufanya kama vile walivyoamuriwa na mufalme, lakini waliwaacha watoto wanaume wa Waisraeli waishi.


Lakini watu wakamwambia Saulo: “Kwa nini Yonatani, aliyeletea Waisraeli ushindi huu mukubwa, auawe? Haiwezikani hata kidogo. Kama vile Yawe anavyoishi, hata unywele mumoja wa kichwa chake hautaanguka chini. Alichokifanya leo, amekifanya kwa musaada wa Yawe.” Kwa hiyo, watu walimukomboa Yonatani naye hakuuawa.


Lakini Petro na Yoane wakawajibu: “Muamue ninyi wenyewe, ni haki mbele ya Mungu kuwatii ninyi kuliko kumutii Mungu?


Mara tu Yehu alipomaliza kutoa sadaka ya kuteketezwa, aliwaambia walinzi na wakubwa: “Muingie muwaue wote. Musimwache hata mumoja atoroke!” Wakaingia na panga zao tayari na kuwaua wote, kisha wakatoa maiti zao inje. Halafu wakaingia katika chumba cha ndani cha hekalu,


na wakati Yezebeli alipowaua manabii wa Yawe, Obadia aliwachukua manabii mia moja, akawaficha makumi tano tano ndani ya pango, akakuwa anawapelekea chakula na maji.


Wakati ule, Adonia mwana wa Daudi kutoka muke wake Hagiti, akaanza kujivuna kwamba yeye ndiye atakayekuwa mufalme. Basi, akajitayarishia magari, wapanda-farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Nyuma ya tukio hilo, Abusaloma alijipatia gari, farasi na watu makumi tano wa kumutangulia.


Sasa ufikiri juu ya jambo hili na uamue la kufanya. Jambo hili linaweza kuleta hasara kwa bwana wetu na jamaa yake yote. Yeye ni mutu mubaya na hakuna anayeweza kusema naye.”


Saulo akamwambia: “Kwa nini wewe na Daudi mwana wa Yese, mumenifanyia shauri baya? Kwa nini ulimupatia mikate na upanga, halafu ukamwombea kwa Mungu? Kwa sababu hiyo, leo ameniasi na ananivizia.”


Lakini Saulo akamutupia Yonatani mikuki kusudi amwue. Naye Yonatani akatambua kwamba baba yake alikuwa amekusudia kumwua Daudi.


Samweli aliwaambia: “Hivi ndivyo mufalme wenu atakayewatawala atakavyowatendea: wana wenu atawafanya wakuwe waendeshaji wa magari yake, na wengine kuwa waaskari wapanda-farasi wake, na wengine watapiga mbio mbele ya magari yake.


Angalia siku zinakuja ambapo nitawaua vijana wote wanaume katika jamaa yako na katika ukoo wako, hata hakutakuwa mwanaume yeyote atakayeishi na kuwa muzee.


Lakini mufalme Saulo akamwambia: “Ahimeleki, hakika utauawa, wewe na jamaa yote ya baba yako.”


Pahali pa ngao hizo, mufalme Rehoboamu alitengeneza ngao za shaba na kuziweka chini ya ulinzi wa wachungaji wa mulango wa nyumba ya kifalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite