Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 20:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Hivyo unitendee mema maana umefanya agano nami, mimi mutumishi wako, mbele ya Yawe. Lakini, kama nimefanya kosa basi, uniue wewe mwenyewe. Kwa nini unipeleke kwa baba yako kusudi aniue?”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 20:8
16 Referans Kwoze  

Abusaloma akamujibu: “Nilikutumia ujumbe, ukuje huku kusudi nikutume kwa mufalme, umwulize: ‘Kwa nini niliondoka Gesuri? Ingekuwa bora kwangu kubaki kule.’ Sasa unisaidie nipate kumwona mufalme. Kama nina kosa basi, aniue!”


Kwa sababu Yonatani alimupenda Daudi kama roho yake, alifanya agano naye.


Hao wote wawili, wakafanya agano mbele ya Yawe. Daudi akabaki katika muji wa Horeshi na Yonatani akaenda zake kwenye nyumba.


ninaomba jina langu lisikatiliwe kabisa kutoka katika jamaa yako. Yawe awalipize kisasi waadui zako.”


Kama mimi ni mukosaji au nimefanya kitendo kinachonipasa kuuawa, mimi sikatai kufa. Lakini kama hakuna ukweli wowote katika mashitaki yao juu yangu, hakuna mutu anayeweza kunitoa kwao. Ninaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma.”


Wema na uaminifu zisitengane nawe. Uvifunge katika shingo lako; uviandike ndani ya moyo wako.


Hata nilisema kwa hofu yangu: “Wanadamu wote hawawezi kutumainiwa!”


Watu wamoja wa makabila ya Benjamina na Yuda wakafika pahali Daudi alipokuwa akijificha.


Naomi akawaambia hao wakwe zake wawili: “Murudi kila mumoja kwa mama yake. Ninaomba Yawe awatendee mema kama vile mulivyonitendea mema mimi na wale watu wangu waliokufa.


“Mungu wa miungu ndiye Yawe! Mungu wa miungu ndiye Yawe! Yeye anajua kwa nini tumefanya hivyo. Na Waisraeli wote watajua vilevile! Kama huu ni uasi au ni ukosefu wa imani kwa Yawe basi, yeye aache kutuokoa leo.


Wale watu wakamujibu: “Uzima wenu ni uzima wetu! Kama hamutaifichua siri yetu, Yawe atakapotupa inchi hii, tutakutendea kwa wema na uaminifu.”


Wakati wa kufa kwake ulipokaribia, Yakobo akamwita mwana wake Yosefu, akamwambia: “Sasa, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, weka mukono wako chini ya mapaja yangu, uniahidi kwamba utanitendea kwa wema na uaminifu. Usinizike huku Misri,


Sasa, basi, muniambie kama muko tayari kumutendea bwana wangu kwa wema na uaminifu. Kama sivyo, basi museme, nami nitajua cha kufanya.”


Yonatani akamujibu: “Wazo lile likuwe mbali nawe. Hakika, kama ningejua kwamba baba yangu amekusudia mabaya juu yako nisingekuficha.”


Saulo alipomaliza kuzungumuza na Daudi, Yonatani mwana wa Saulo alivutwa sana na Daudi, akamupenda kwa moyo wake wote kama alivyojipenda yeye mwenyewe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite