Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 2:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 Na litakalowapata watoto wako wawili, Hofuni na Finehasi, ni hili: Wote wawili watakufa siku moja. Hiki kitakuwa ni kitambulisho kwako.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 2:34
10 Referans Kwoze  

Mutu huyo akaonyesha kitambulisho siku ileile, akasema: “Hiki ndicho kitambulisho Yawe alichosema: ‘Mazabahu hii itabomoka, na majivu yanayokuwa juu yake yatamwangika.’ ”


Sanduku la Agano la Mungu lilitekwa, na wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi, wakauawa.


Yule aliyeleta habari akasema: “Waisraeli wamewakimbia Wafilistini. Kumekuwa mauaji makubwa kati ya Waisraeli. Zaidi ya yote, wana wako wote wawili, Hofuni na Finehasi, wameuawa, na Sanduku la Agano la Mungu limetekwa.”


Ahiya akamwambia muke wa Yeroboamu: “Simama, urudie kwako sasa. Mara tu utakapoingia katika muji, mwana wako atakufa.


Siku hiyo, nitatimiza yale yote niliyosema tangu mwanzo mpaka mwisho juu ya Eli na juu ya jamaa yake.


Na hiki ndicho kitambulisho kwenu: mutamukuta mutoto muchanga amefunikwa nguo za kitoto, naye amelalishwa katika sanduku ya kukulishia nyama.”


Mutu wako ambaye sitamwangamiza kutoka mazabahu yangu atakuwa ameponyoka kusudi nipofushe macho yake, naye atakufa moyo na wazao wake watauawa kifo kibaya.


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Naye akamwita mutoto wake Ikabodi, maana alisema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli”, akiwa na maana kwamba Sanduku la Agano lilikuwa limetekwa, tena baba mukwe wake na mume wake, wote walikufa.


Akasema: “Utukufu wa Mungu umeondolewa kwa Waisraeli maana Sanduku la Agano la Yawe limetekwa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite