Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 2:3
26 Referans Kwoze  

Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.


basi, usikilize kule kwako mbinguni, uwasamehe na kumutendea kila mutu kwa kadiri anavyostahili, maana ni wewe tu unayejua mawazo ya mioyo ya wanadamu wote,


Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!


Kwa maana Neno la Mungu ni lenye uzima, na lina nguvu; ni kali kupita upanga unaokata ngambo mbili. Linapenya hata linatenga moyo na roho na hata viungo na ubongo. Nalo linatambua nia na mawazo ya mutu.


Matendo yote ya mutu yanaonekana kwake kuwa sawa lakini Yawe anapima nia ya mutu.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Bwana wetu ni mukubwa, ana nguvu nyingi; maarifa yake hayana kipimo.


Mpaka wakati gani waovu watajigamba kwa maneno? Watajivuna na kujitapa mpaka wakati gani?


Tungalikuwa tumekusahau wewe Mungu wetu, na kumukimbilia mungu wa uongo,


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Yawe anasema hivi: Maneno yenu yamekuwa muzigo kwangu. Hata hivyo munasema: Tumesema nini juu yako?


TEKELI: wewe umepimwa kwenye mizani, nawe ukaonekana hauna uzito wowote.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Hao hawana huruma yoyote ndani ya moyo; wamejaa maneno ya kujivuna.


Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.


Ninawaambia wenye kiburi: ‘Mwache kiburi’, na waovu: ‘Musiote mapembe!


“Mungu wa miungu ndiye Yawe! Mungu wa miungu ndiye Yawe! Yeye anajua kwa nini tumefanya hivyo. Na Waisraeli wote watajua vilevile! Kama huu ni uasi au ni ukosefu wa imani kwa Yawe basi, yeye aache kutuokoa leo.


Kisha Zebuli akamwambia: “Majivuno yako yako wapi sasa? Si ni wewe uliyesema: ‘Abimeleki ni nani? Kwa nini tumutumikie?’ Sasa, hao ndio watu uliowazarau. Kwenda upigane nao.”


Nimesikia jinsi unavyojivuna na kusema maneno mengi juu yangu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite