Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 2:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Kati ya makabila yote ya Israeli nilimuchagua Haruni na jamaa yake kuwa makuhani wangu, wanitumikie kwenye mazabahu, wafukize ubani na kuvaa kizibao mbele yangu. Nikaipatia jamaa ya babu yako sadaka zangu ambazo Waisraeli walinitolea kwa moto.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 2:28
26 Referans Kwoze  

Nawe Musa umulete kwangu Haruni ndugu yako, pamoja na wana wake: Nadabu, Abihu, Eleazari na Itamari. Utawachagua kati ya Waisraeli, kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Ninakupa wewe, wana wako na wabinti zako, vitu vyote ambavyo watu wa Israeli wananitolea; hivyo ni haki yenu siku zote. Hili ni agano la milele mbele yangu ambalo ni kwa ajili yako na wazao wako.


Sadaka yoyote ya ngano iliyotolewa na kuhani itateketezwa yote; haitakuliwa hata kidogo.


Sehemu inayobaki ya sadaka ya ngano, ni ya makuhani. Hiyo ni sehemu takatifu kabisa ya sadaka inayotolewa Yawe kwa moto.


Sehemu inayobaki ya sadaka hiyo ni ya makuhani. Hiyo ni sehemu takatifu kabisa ya sadaka Yawe anayotolewa kwa moto.


Uwaambie wamutengenezee vitu hivi: kifuko cha kifua, kizibao, kanzu, na ingine yenye kupambwa vizuri, kofia na mukaba. Ndugu yako Haruni na wana wake watavaa nguo zile kusudi wanitumikie kama vile makuhani.


Natani akamwambia Daudi: “Wewe ndiwe mutu yule! Sasa, Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Mimi nilikupakaa mafuta ukuwe mufalme juu ya Israeli. Nilikuokoa toka katika mikono ya Saulo.


Kisha akamwambia Kora na wafuasi wake: Kesho asubui, Yawe ataonyesha ni nani anayekuwa wake na ni nani anayekuwa mutakatifu, na yule atakayemuchagua, atamuwezesha kukaribia kwenye mazabahu.


Muguu wa kuume wa nyuma wa nyama wa sadaka zenu za amani mutamupa kuhani.


Kila siku Haruni anapoingia kwa kutayarisha taa zinazokuwa pale, atafukiza ubani wenye harufu nzuri juu ya mazabahu hiyo.


Tena atafukiza ubani wakati wa magaribi anapowasha taa. Sadaka hii ya ubani itatolewa siku zote bila kukoma katika vizazi vyenu vyote.


Walipotakaswa kwa kupakwa mafuta, Yawe aliamuru Waisraeli wawape sehemu hiyo ya sadaka; hiyo itakuwa siku zote haki yao.


Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.


Ahiya mwana wa Ahitubu ndugu yake na Ikabodi mwana wa Finehasi mujukuu wa Eli kuhani wa Yawe katika muji wa Shilo, alikuwa ndiye aliyevaa kizibao cha kuhani. Watu hawakujua kwamba Yonatani amekwisha ondoka.


Daudi alikuwa amejifungia kizibao cha kuhani katika kiuno chake. Alicheza kwa nguvu zake zote mbele ya Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite