Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 2:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 2:25
25 Referans Kwoze  

Kwa maana tukifanya zambi kwa makusudi tukisha kutambua waziwazi ukweli, hakuna tena sadaka ingine inayoweza kutolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu.


Kwa hiyo ninaapa juu ya jamaa ya Eli kwamba uovu wao hautaondolewa hata kidogo kwa matoleo wala kwa sadaka.”


Ilikuwa ni mapenzi ya Yawe mwenyewe kuifanya mioyo ya watu wa mataifa hayo kuwa migumu kusudi wapigane. Alikusudia wasihurumiwe lakini wateketezwe. Ndivyo Yawe alivyomwamuru Musa.


Lakini mutu yeyote atakayekosa kwa makusudi, akuwe mwanainchi au mugeni, atakuwa amemutukana Yawe, na anapaswa kutengwa mbali kati ya watu wake.


Azabu kali ni kwa wanaoacha mwenendo mwema; yeyote anayechukia kuonywa atakufa.


Kwa maana kuna Mungu mumoja tu, na kuna mupatanishi mumoja tu kati ya Mungu na watu, ni yule mutu, Kristo Yesu,


Ni kwa sababu hii anaweza kuwaokoa kabisa wao wanaokuja kwa Mungu kwa njia yake, kwa maana yeye anaishi siku zote kusudi akuwe mwombezi mbele ya Mungu.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Na alipokuwa angali akisema naye, Amazia akamwambia: “Nyamaza! Tulikufanya wewe kuwa mushauri wa mufalme? Kwa nini uawe?” Nabii akanyamaza, lakini akasema: “Ninafahamu kwamba Mungu ameamua kukuangamiza kwa maana umetenda haya yote, kisha unazarau shauri langu.”


Musipendelee mutu yeyote katika kutoa hukumu; mutawasikiliza bila upendeleo, wakubwa kwa wadogo. Musiogopeshwe na sura ya mutu, maana ninyi mutapaswa kuhukumu kwa ajili ya Mungu. Kukikuwa maneno ambayo ni magumu sana kwenu, mutayafikisha kwangu nami nitayasikiliza.’


Uniokoe kutoka kosa la kumwanga damu, ee Mungu, Mungu mwokozi wangu, nami nitaimba kwa sauti kwamba umeniokoa.


“Lakini Sihoni, mufalme wa Hesiboni, hakuturuhusu tupite katika inchi yake. Yawe, Mungu wenu, akamufanya akuwe na kichwa kigumu na mugumu wa moyo, kusudi tumushinde na kutwaa inchi yake ambayo tunairizi mpaka leo.


Lakini inayobaki tu ni kungojea kwa woga hukumu na moto mukali wa Mungu utakaowateketeza waasi.


Hakuna mwamuzi kati yetu ambaye angetuamua sisi wawili.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Lakini Eri, muzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu mbele ya Yawe, hivyo Yawe akamwua.


Tendo hilo likamwuzi Yawe, akamwua Onani vilevile.


“Mutu akimukosea mwenzake, naye akiletwa apate kuapa mbele ya mazabahu yako katika nyumba hii, naye akiapa,


tafazali wewe usikilize kutokea kule mbinguni, utende na kuwahukumu watumishi wako. Anayekuwa na kosa umwazibu kwa kadiri ya makosa yake; asiyekuwa na kosa umwachilie na kumupatia haki kwa kadiri ya haki yake.


Halafu mufalme hakuwajali watu kwa sababu jambo hili lilisababishwa na Mungu kusudi Yawe atimize neno lake alilomwambia Yeroboamu, mwana wa Nebati kwa njia ya Ahiya wa Shilo.


Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite