Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 2:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Zambi hii ya vijana hao wa Eli ilikuwa kubwa sana mbele ya Yawe. Maana, vijana hao walizarau matoleo ya Yawe.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 2:17
11 Referans Kwoze  

Zaidi ya hayo yote, munaifunika mazabahu ya Yawe kwa machozi yenu, mukilia na kuomboleza kwa sababu yeye hazikubali tena sadaka munazomutolea.


Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Mungu aliona kwamba dunia imeharibika na kujaa mateso makali.


Ole kwa dunia kwa ajili ya vikwazo vinavyokuwa ndani yake! Vikwazo haviwezi kosa kutokea, lakini ole kwa mutu yule anayevileta!


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Unisafishe kabisa kosa langu; unitakase zambi yangu.


Naye alimutoa mwana wake kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Alipiga ramuli; aliaguza akishirikiana na waaguzi wanaosemezana na mizimu na wachawi. Alitenda maovu mengi mbele ya Yawe, akamukasirikisha.


Alikuwa mwindaji shujaa mbele ya Yawe, ndiyo maana kuna musemo unaosema: “Kama vile Nimurodi mwindaji shujaa mbele ya Yawe.”


Na kama mutu huyo akimujibu: “Ngojea kwanza niteketeze mafuta halafu utakamata kadiri unataka”, hapo huyo mutumishi wa kuhani anamujibu: “Hapana, unapaswa kunipatia sasa hivi. Kama sivyo, nitaitwaa kwa nguvu.”


Nimekwisha kumwambia kwamba nitaiazibu jamaa yake milele, kwa uovu anaoujua kwa sababu wana wake wamenikufuru mimi na hakuwazuia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite