Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 2:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Zaidi ya hayo, hata mbele mafuta hayajateketezwa kwa moto, mutumishi wa kuhani anakuja na kumwambia yule mutu anayetolea sadaka: “Mumutoshee kuhani nyama ya kuchoma maana yeye hatapokea nyama yako iliyotokoteshwa, lakini inayokuwa mbichi.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 2:15
8 Referans Kwoze  

Kuhani ataviteketeza juu ya mazabahu kama chakula kinachotolewa kwa Yawe kwa moto kutoa harufu ya kumupendeza Mungu. Mafuta yote ni ya Yawe.


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Kwa maana watu wa namna hii hawamutumikii Bwana wetu Kristo, lakini wanatumikia tu tumbo yao wenyewe. Tena kwa maneno yao matamu na ya kujipendekeza wanadanganya watu wasiokuwa na makosa.


Kufika kwao kunaleta machafuko katika karamu zenu za upendo. Wanakula na kushiba pamoja nanyi pasipo haya yoyote. Wao ni kama mawingu yanayopeperushwa na upepo pasipo kuleta mvua. Wao ni kama miti isiyozaa matunda hata wakati wa mavuno; ni miti iliyoongolewa na kufa kabisa.


Imekatazwa kuikula ikiwa mbichi au imetokoteshwa kwa maji, lakini inapaswa kuchomwa yote, pamoja na kichwa, miguu na nyama zake za ndani.


huyo mutumishi alichomeka kanya ile ndani ya chungu, nyama yoyote inayonyanyuliwa na kanya ile ilikuwa mali ya kuhani. Waisraeli wote waliokwenda Shilo kutolea sadaka zao walitendewa hivyo.


Na kama mutu huyo akimujibu: “Ngojea kwanza niteketeze mafuta halafu utakamata kadiri unataka”, hapo huyo mutumishi wa kuhani anamujibu: “Hapana, unapaswa kunipatia sasa hivi. Kama sivyo, nitaitwaa kwa nguvu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite