Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 19:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yonatani alimusifu Daudi mbele ya baba yake, akamwambia: “Usitende zambi juu ya mutumishi wako Daudi maana yeye hajatenda zambi yoyote juu yako. Matendo yake yote siku zote yamekuwa mazuri kwako.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 19:4
15 Referans Kwoze  

Mutu analipwa mabaya kwa mema? Lakini, wamenichimbia shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele yako, nikasema mema kwa ajili yao, kusudi niepushe hasira yako mbali nao.


Rubeni akawaambia: “Si niliwaambia tusimuzuru kijana? Lakini ninyi hamukunisikiliza! Sasa tunaazibiwa kwa ajili ya damu yake.”


Mwenye kulipa mazuri kwa mabaya, mabaya hayataondoka katika nyumba yake.


Yonatani akamujibu: “Kwa nini auawe? Amefanya nini?”


Wananilipa mabaya kwa mazuri; nami pekee nimebaki ukiwa.


Ahimeleki akamujibu: “Kati ya watumishi wako, Daudi ndiye mukubwa wa kuaminika kuliko wote. Yeye ni mukwe wako wewe mufalme mwenyewe, mukubwa wa waaskari wako walinzi na anaheshimiwa kuliko wote katika nyumba yako.


Kwa kuwakosesha wandugu zenu kama hivi na kuumiza zamiri yao, ni kama vile munamukosea Kristo mwenyewe.


“Mutu akimukosea mwenzake, naye akiletwa apate kuapa mbele ya mazabahu yako katika nyumba hii, na akiapa tafazali


Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.


Anayemwanga damu ya mwanadamu, damu yake itamwangwa na mwanadamu; maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.


Kila mutu anayemuchukia ndugu yake ni mwuaji, nanyi munajua kwamba mwuaji yeyote hana uzima wa milele ndani yake.


Angalia! Wananivizia waniue. Watu wakali wanachochea ugomvi juu yangu ingawa sikufanya ubaya wowote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite