Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 19:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Daudi alipotoroka, alikwenda Rama kwa Samweli. Alimwelezea Samweli mambo yote aliyomufanyia Saulo. Basi, Daudi na Samweli walikwenda na kukaa kule Nayoti.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 19:18
11 Referans Kwoze  

Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana kule ndiko kulikuwa kwake. Aliwaamulia Waisraeli haki zao kule, na kumujengea Yawe mazabahu kule.


Basi muitikiane zambi ninyi kwa ninyi na kuombeana kusudi mupate kuponyeshwa. Maombi ya bidii ya mwenye haki ni yenye faida kubwa.


Hata nilisema kwa hofu yangu: “Wanadamu wote hawawezi kutumainiwa!”


Wakati ule, Samweli alikuwa amekwisha kufa, na Waisraeli wote walikuwa wamekwisha kumwombolezea na kumuzika katika muji wake Rama. Saulo alikuwa amewafukuza kutoka katika inchi wenye kutabiri na wachawi.


Kisha, Samweli akaenda Rama; na mufalme Saulo akarudi kwenye nyumba yake kule Gibea.


Kisha Saulo aliambiwa kwamba Daudi yuko kule Nayoti katika muji wa Rama.


Kwa hiyo yeye mwenyewe akaenda Rama. Alipofika kwenye kisima kikubwa kinachokuwa kule Seku, akamukuta mutu fulani ambaye alimwuliza: “Samweli na Daudi wako wapi?” Yule mutu akamujibu: “Wako Nayoti, katika muji wa Rama.”


Naye Saulo akaenda kule Nayoti katika muji wa Rama. Alipofika kule, Roho wa Mungu akamufikia, naye alianza kutabiri akiwa katika njia mpaka alipofika Nayoti katika muji wa Rama.


Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.


Daudi alikimbia kutoka Nayoti katika Rama, akaenda mpaka kwa Yonatani, akamwambia: “Nimefanya nini? Kosa langu ni gani? Nimemutendea baba yako zambi gani hata anajaribu kuyaangamiza maisha yangu?”


Siku hiyo, Daudi alimukimbia Saulo, akaenda kwa mufalme Akisi wa Gati.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite