Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 19:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Saulo alijaribu kumuchoma Daudi kwa mukuki ule. Lakini Daudi aliepa mukuki wa Saulo na mukuki ukapiga ukuta. Daudi akakimbia na kutoroka.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 19:10
20 Referans Kwoze  

Lakini Saulo akamutupia Yonatani mikuki kusudi amwue. Naye Yonatani akatambua kwamba baba yake alikuwa amekusudia kumwua Daudi.


Basi, alimutupia Daudi mukuki mara mbili maana alifikiri: “Nitamubanisha Daudi kwenye ukuta.” Lakini Daudi aliepa mara zote mbili.


Hakuna hekima, ufahamu, wala shauri yoyote ya mutu, itakayoweza kupingana na Yawe.


Wakajaribu tena kumufunga Yesu, lakini akawaponyoka.


Lakini yeye akapita katikati yao, na kujiendea.


Watakapowatesa katika muji mumoja, mukimbilie katika muji mwingine. Kweli ninawaambia: hamutamaliza kuzunguka katika miji yote ya Israeli mbele ya kurudi kwa Mwana wa Mutu.


Lakini Yawe anasema hivi: Nitakutendea nini, ee Efuraimu? Nikufanyie nini, ee Yuda? Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi.


Silaha zote zilizotengenezwa kwa kukuzuru wewe hazitafaa kwa kitu chochote. Mutu akikushitaki, utamushinda. Hiyo ndiyo haki niliyowapangia watumishi wangu. Hizo ndizo haki nilizowahakikishia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Tumeponyoka kama ndege katika mutego; mutego umefyatuka, nasi tukaponyoka.


Yawe ni karibu na wenye kuvunjika moyo; anawaokoa wote waliokata tamaa kabisa.


Mungu alinyoosha mukono wake kutoka juu, akanitwaa, alininyanyua kutoka ndani ya maji mengi.


Saulo alimusikiliza Yonatani, kisha akaapa: “Kama vile Yawe anavyoishi, sitamwua Daudi.”


walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.


Maana wao wako mbio kutenda maovu, haraka zao zote ni za kumwanga damu.


Kesho yake, pepo muchafu kutoka kwa Mungu akamushambulia Saulo kwa rafla, akakuwa anapayukapayuka kama mwenda-wazimu katika nyumba yake. Daudi alikuwa anapiga kinubi kama alivyofanya siku zote. Saulo alikuwa na mukuki katika mukono wake.


Mutu mwovu anamuvizia mutu wa haki, na kujaribu kumwua;


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite