Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 18:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Saulo akawaambia: “Mumwambie Daudi hivi: ‘Kile ambacho mufalme anataka kama vile mali kwa binti yake ni magovi mia moja ya Wafilistini, kusudi ajilipize kisasi kwa waadui zake.’ ” Hivi ndivyo Saulo alivyopanga kusudi Daudi auawe na Wafilistini.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 18:25
13 Referans Kwoze  

Saulo akamwambia Daudi: “Huyu ni Merabu, binti yangu mukubwa, nitamutoa kwako kusudi umwoe kwa masharti mawili: Ukuwe askari wangu shujaa na mutiifu, upigane vita ya Yawe.” Saulo alizani kwa njia hiyo Wafilistini watamwua Daudi, kusudi kitendo hicho asikifanye yeye mwenyewe.


Siku ile, Waisraeli walisumbuliwa sana maana Saulo alikuwa amewaapiza watu akisema: “Alaaniwe mutu yeyote atakayekula chakula mbele jua kutua, na mbele sijajilipiza waadui zangu kisasi.” Kwa hiyo, siku yote, hakuna mutu aliyeonja chakula chochote.


Muniombe mali na zawadi, hata ikiwa kikubwa namna gani, nami nitatoa, kufuatana na jinsi mutakavyoniambia. Lakini munipatie tu binti huyu kuwa muke wangu.”


Mimi mutumishi wako nimekwisha kuua simba wengi na dubu wengi. Sasa, hata yule Mufilistini mupagani, ambaye amewatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima, atakuwa kama wao.


Daudi akawauliza wale waliokuwa karibu naye: “Mutu atakayemwua Mufilistini huyu na kuikomboa Israeli kutokana na haya hii atafanyiwa nini? Ni nani huyu Mufilistini, mutu mupagani, anayesubutu kuwatukana waaskari wa Mungu Mwenye Uzima?”


Basi, Yoshua akatengeneza visu hivyo vya jiwe gumu na kuwatahiri Waisraeli kule Gibea-Haraloti.


Yakobo akamupenda Rakeli; kwa hiyo akamwambia Labani: “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Rakeli, binti yako mudogo.”


Wale watumishi walimwelezea Saulo kama vile Daudi alivyosema.


Daudi vilevile alituma wajumbe kwa Isiboseti mwana wa Saulo akisema: “Unirudishie muke wangu Mikali ambaye nilimwoa kwa magovi mia moja ya Wafilistini.”


Saulo alimwelezea mwana wake Yonatani na wakubwa wake juu ya mupango wake wa kumwua Daudi. Lakini Yonatani, mwana wa Saulo, alimupenda sana Daudi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite