Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 18:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Basi, watumishi hao wa Saulo walimwambia Daudi maneno hayo kwa siri, naye akawaambia: “Munazani mufalme kuwa baba mukwe wangu ni jambo dogo? Mimi ni mutu masikini na wa hali ya chini.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 18:23
12 Referans Kwoze  

Muangalie namna Baba alivyoonyesha upendo wake kwetu hata tupate kuitwa watoto wa Mungu! Na kwa hakika sisi ndio wao! Ndiyo maana watu wa dunia hawatutambui, kwa sababu hawakumujua Mungu.


Masikini anachukiwa hata na jirani yake, lakini tajiri ana warafiki wengi.


Mimi ni mudogo na ninazarauliwa; hata hivyo sisahau kanuni zako.


Saulo akajibu: “Mimi ni wa kabila la Benjamina, kabila dogo kuliko makabila yote ya Waisraeli. Na katika kabila lote la Benjamina jamaa yangu ndiyo ndogo kabisa. Lakini, kwa nini unanizungumuzia namna hiyo?”


Basi, Yakobo akamutumikia Labani miaka saba kwa ajili ya Rakeli, lakini kwake muda ule ulikuwa kama siku chache, kwa vile alivyomupenda Rakeli.


Muniombe mali na zawadi, hata ikiwa kikubwa namna gani, nami nitatoa, kufuatana na jinsi mutakavyoniambia. Lakini munipatie tu binti huyu kuwa muke wangu.”


Daudi akamwambia Saulo: “Mimi ni nani hata mufalme akuwe baba mukwe wangu? Ukoo wangu wenyewe na hata jamaa ya baba yangu si kitu katika Israeli.”


Halafu Saulo aliwaamuru watumishi wake akisema: “Museme na Daudi kwa siri na kumwambia: ‘Mufalme anapendezwa sana nawe, hata watumishi wake vilevile wote wanakupenda’. Hivyo, sasa ukubali kuwa mukwe wa mufalme.”


Wale watumishi walimwelezea Saulo kama vile Daudi alivyosema.


Mwenye kumubembeleza jirani yake, anatega mutego wa kujinasa mwenyewe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite