Kisha mufalme Daudi akaingia ndani na kuikaa mbele ya Yawe; halafu akaomba: “Mimi ni nani, ee Bwana wangu Yawe, na jamaa yangu ni nini hata ukaniinua mpaka hapa ninapokuwa leo!
Basi, watumishi hao wa Saulo walimwambia Daudi maneno hayo kwa siri, naye akawaambia: “Munazani mufalme kuwa baba mukwe wangu ni jambo dogo? Mimi ni mutu masikini na wa hali ya chini.”
Saulo akajibu: “Mimi ni wa kabila la Benjamina, kabila dogo kuliko makabila yote ya Waisraeli. Na katika kabila lote la Benjamina jamaa yangu ndiyo ndogo kabisa. Lakini, kwa nini unanizungumuzia namna hiyo?”
Hapo Ruta akamwinamia Boazi uso mpaka chini kwa unyenyekevu, akamwambia: “Nimepata namna gani kukubaliwa mbele yako? Mbona unanishugulikia ijapokuwa mimi ni mugeni tu?”