Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 17:52 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

52 Halafu watu wa Israeli na watu wa Yuda walianza kupiga kelele za ushindi, wakawafuatilia Wafilistini mpaka Gati, kwenye milango ya muji wa Ekroni, hata Wafilistini walioumizwa katika vita walikufa katika njia tangu Saraimu mpaka Gati na Ekroni.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 17:52
10 Referans Kwoze  

Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekuroni, ukazunguka kuelekea Sikeroni ambapo ulipita karibu na mulima Bala mpaka Yabuneli ukaishia katika bahari ya Mediteranea.


Lakini Eleazari alisimama imara na kupigana na Wafilistini mpaka mukono wake uliposhindwa kupindika, ukabaki umebania upanga wake. Siku hiyo, Yawe alijipatia ushindi mukubwa. Nyuma ya ushindi ule, Waisraeli walirudi pahali Eleazari alipokuwa na kuteka vitu kutoka kwa Wafilistini waliouawa.


Waisraeli wa kabila la Nafutali, Aseri, na Manase, wote waliitwa, wakawafuatilia Wamidiani.


Waisraeli walipotoka kuwafuatilia Wafilistini, waliteka vitu ndani ya kambi yao.


Walituma wajumbe na kuwakusanya wakubwa wote wa Wafilistini na kuwauliza: “Tutafanya nini na Sanduku hili la Mungu wa Israeli?” Wakubwa wao wakajibu: “Sanduku hilo la Mungu wa Israeli mulipeleke Gati.” Basi, wakalipeleka kwenye muji wa Gati.


Hivyo, wakalipeleka Sanduku hilo la Mungu kwenye muji wa Ekuroni. Lakini Sanduku hilo la Mungu lilipofika kule, watu wa muji huo walipiga kelele: “Wametuletea Sanduku la Mungu wa Israeli kwa kutuua sisi na watu wetu.”


Basi, mufalme wa Israeli akashinda vita, akateka farasi na magari ya vita mengi, na kuwaua Waaramu kwa wingi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite