Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 17:43 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

43 Goliati akamwuliza Daudi: “Sasa, hiyo fimbo ni ya nini? Unazani mimi ni imbwa hata unifikie kwa fimbo?” Mufilistini yule akamulaani Daudi kwa miungu yake.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 17:43
14 Referans Kwoze  

Mefiboseti akainama, na kusema: “Mimi ni sawa na imbwa mufu. Kwa nini unishugulikie hivyo?”


Abeneri alikasirika sana kutokana na maneno ya Isiboseti, akasema: “Unafikiri mimi ni imbwa anayeitumikia jamaa ya Yuda? Angalia, mimi nimewatendea mema jamaa ya baba yako Saulo, wandugu zake, na warafiki zake na sikukutoa kwa Daudi mpaka leo. Hata hivyo, leo hii unaniona kuwa mwenye kosa kwa ajili ya mwanamuke.


Kumbuka mezali ya kale inayosema ‘Uovu unatoka ndani ya mwovu’, lakini sitanyoosha mukono juu yako.


Kama vile ndege anavyorukaruka, vilevile laana isiyokuwa na sababu haimupati mutu.


Hazaeli akauliza: “Lakini mimi mutumishi wako ni kitu kweli? Mimi ninayekuwa sawa na imbwa nitaweza namna gani kutenda mambo hayo makubwa?” Elisha akamujibu: “Yawe amenionyesha kwamba utakuwa mufalme wa Aramu.”


Kwa hiyo, Abisayi mwana wa Zeruya akamwambia mufalme: “Kwa nini huyu anayekuwa sawa imbwa mufu akulaani wewe bwana wangu mufalme? Uniruhusu nimwendee, nami nitakikata kichwa chake.”


Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”


Kuja sasa uwalaani watu hawa kwa ajili yangu maana wana nguvu kuliko mimi. Labda nitaweza kuwashinda na kuwafukuza wasiingie katika inchi yangu, kwa maana unajua kwamba wewe ukimubariki mutu anabarikiwa, ukimulaani mutu analaaniwa.


Wakatoka na kwenda kwenye mashamba yao ya mizabibu, wakachuma zabibu halafu wakazikamua, wakatengeneza divai wakafanya sikukuu. Wakaingia kwenye nyumba ya mungu wao wakakula na kunywa, kisha wakamutukana Abimeleki.


Wafilistini waliokuwa kwenye kambi wakamwita Yonatani na kijana aliyemubebea silaha: “Mukuje huku kwetu, nasi tutawaonyesha kitu.” Yonatani akamwambia yule kijana aliyemubebea silaha: “Unifuate. Yawe amewatia katika mikono ya Waisraeli.”


Wakati Daudi alipofika kule Bahurimu, kulitokea mutu mumoja wa ukoo wa Saulo, jina lake Simei mwana wa Gera, akaanza kumulaani Daudi kwa mufululizo.


Beni-Hadadi akamutumia Ahabu ujumbe huu: “Miungu iniue ikiwa kule Samaria kutabakia mavumbi ya kutosha kwa kujaza vitanga vya mikono kwa kila mumoja wa watu wangu wengi wanaonifuata!”


Sasa wewe mufalme wa Israeli angalia mutu unayetaka kumwua! Unamufuatilia nani? Unafuatilia imbwa yenye kufa! Unakifuatilia kiroboto!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite