Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 15:32 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

32 Kisha Samweli akasema: “Muniletee hapa Agagi mufalme wa Waamaleki.” Agagi akamwendea Samweli akiwa mwenye furaha maana alifikiri: “Uchungu wa kifo umepita.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 15:32
8 Referans Kwoze  

Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Atakayetoroka kitisho atatumbukia ndani ya shimo; atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Kwa maana nitaleta mambo hayo juu ya Moabu, katika mwaka wao wa azabu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Basi, Samweli akarudi pamoja naye mpaka Gilgali na Saulo akamwabudu Yawe.


Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.


Ndiyo maana ninawashambulia kwa njia ya manabii, nimewaangamiza kwa maneno yangu, hukumu yangu inajitokeza kama mapambazuko.


Kisha Yoshua akasema: “Mufungue mulango wa pango muniletee kutoka mule wale wafalme watano.”


Gideoni akafuata njia ya upande wa magaribi inayokuwa upande wa mashariki wa Noba na Yogibeha, akalishambulia jeshi hilo ambalo halikukuwa tayari.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite