Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 15:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 “Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 15:11
44 Referans Kwoze  

Samweli akamujibu Saulo: “Umefanya kipumbafu. Haukutii mambo Yawe, Mungu wako, aliyokuamuru. Kama ungetii, Yawe angeudumisha milele ufalme wako juu ya Israeli.


Yawe akasikitika sana kwa kumwumba mwanadamu katika dunia. Yawe akahuzunika sana ndani ya moyo wake.


Macho yangu yanatiririka machozi kama muto, kwa sababu watu hawaishiki sheria yako.


Lakini wakati malaika aliponyoosha mukono wake kuelekea Yerusalema kwa kuuangamiza, Yawe alibadilisha nia yake. Yawe akamwambia yule malaika aliyetimiza maangamizi kwa watu: “Basi! Inatosha; rudisha mukono wako.” Malaika wa Yawe alikuwa amesimama karibu na kiwanja cha kupepetea ngano cha Arauna wa muji wa Yebusi.


Kilio hiki kinasikilika Sayuni: Tumeangamia kabisa! Tumefezeheshwa kabisa, kwa maana sherti tuiache inchi yetu, nazo nyumba zetu zibomolewe!


Mwovu anajipendelea mwenyewe, anafikiri uovu wake hautagunduliwa na kulaaniwa.


Tangu siku ile, Samweli hakumwona tena Saulo, mpaka siku alipokufa. Hata hivyo Samweli alimulilia Saulo. Naye Yawe alisikitika kwamba alikuwa amemusimika Saulo kuwa mufalme juu ya inchi ya Israeli.


Lakini Saulo na watu wake hawakumwua Agagi, kondoo bora kabisa, ngombe wazuri, wana-ngombe, wana-kondoo na chochote kile kilichokuwa kizuri hawakukiangamiza. Lakini vitu vyote vibaya na visivyokuwa vya bei kali waliviangamiza.


Sasa, uende kushambulia na kuangamiza vitu vyote wanavyokuwa navyo. Usiwaache wazima, lakini uwaue wote: wanaume kwa wanawake, watoto wachanga na wenye kunyonya, ngombe, kondoo, ngamia na punda.’ ”


Mwenye haki mbele yangu ataishi kwa njia ya imani. Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”


Lakini mimi ninawaambia: muwapende waadui zenu na muwaombee wale wanaowatesa.


Na kama musiponisikiliza, moyo wangu utalia machozi kwenye uficho, kwa sababu ya kiburi chenu. Nitalia kwa uchungu na kutoa machozi, maana watu wa Yawe wanapelekwa katika uhamisho.


Heri ningepata kibanda cha wasafiri katika jangwa, ningewaacha watu wangu na kujiendea. Wote ni wazinzi, ni kundi la watu waasi.


Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya, uwatoweshe pamoja na watenda maovu. Amani ikuwe na Israeli!


Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”


Ingawa niliwapenda, walinishitaki. Hata hivyo, niliwaombea.


Lakini waligeuka na kufanya mabaya kama babu zao; wakayumbayumba kama upinde usiokuwa imara.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


“Watu wote wa Yawe wanauliza hivi: ‘Ni udanganyifu gani huu mumemufanyia Mungu wa Israeli? Mbona mumemwasi Yawe kwa kujenga mazabahu hii?


Katika siku zile, Yesu akapanda juu ya kilima kwenda kuomba na kukesha usiku wote akiomba Mungu.


Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Yawe, wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.


Kwa hiyo akaomba: Yawe, si hayo ndiyo mambo yaleyale niliyowaza utayafanya nilipokuwa katika inchi yangu? Ndiyo maana nilifanya haraka kukimbilia Tarsisi. Nilijua kwamba wewe ni Mungu ambaye umejaa huruma na rehema, haukasiriki upesi, wewe ni mwingi wa wema, na tayari kubadilisha nia yako kusudi usiazibu.


Mungu alipoona walivyofanya, na jinsi walivyouacha uovu wao, akabadilisha nia yake, akaacha kuwatenda kama alivyokuwa amekusudia.


Basi, Bwana wetu Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Halitatukia!


Hivyo akasema: “Nitamuharibu kabisa katika dunia mwanadamu niliyemwumba, pamoja na nyama wa pori, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Ninasikitika kwamba niliwaumba katika dunia.”


Lakini Musa akamusihi Yawe, Mungu wake, akisema: Ee Yawe, kwa nini hasira yako inawaka vikali juu ya watu wako uliowatoa katika inchi ya Misri kwa uwezo mukubwa na mukono wenye nguvu?


Basi, Yawe akaacha kuwafanyia watu wake lile jambo baya alilokuwa amesema.


Lakini jambo la Waisraeli la kutaka wapewe mufalme wa kuwatawala, halikumupendeza Samweli. Naye akamwomba Yawe.


Neno la Yawe lilimufikia Samweli kusema hivi:


Halafu Mungu akatuma malaika aende kuharibu Yerusalema. Lakini mbele hajafanya vile, Yawe akageuza nia yake na kumwambia malaika yule aliyetimiza maangamizi: “Basi, inatosha!” Malaika alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupepetea ngano wa Ornani wa kabila ya Yebusi.


kwa sababu wameacha kumufuata yeye, wakazarau njia zake zote.


Wameurudilia uovu wa babu zao ambao walikataa kusikiliza maneno yangu; wanaiabudu miungu mingine na kuitumikia. Watu wa Israeli na watu wa Yuda wamevunja agano nililofanya na babu zao.


Lakini muligeuka, mukachafua jina langu, wakati mulipowakamata tena watumwa na wajakazi walewale ambao mulikuwa mumewaachilia kama walivyotaka, mukawalazimisha kuwa watumwa tena.


Lakini, mutu wa haki akiacha haki yake na kutenda uovu na kufanya machukizo yaleyale mutu mwovu anayofanya, basi, huyo ataishi? Hapana! Matendo yake yote mema aliyotenda hayatakumbukwa tena; atakufa kwa sababu ya uasi na zambi aliyotenda.


Yawe akamwambia Samweli: “Utamulilia Saulo mpaka wakati gani? Wewe unajua kwamba mimi nimemukataa kuwa mufalme wa Israeli. Sasa, jaza ile pembe yako ya kuwekea mafuta, uondoke. Nitakutuma kwa Yese wa muji wa Betelehemu. Maana nimejipatia mufalme kati ya wana wake.”


Basi, Yawe alimukasirikia Solomono, kwa sababu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa Israeli, ingawa yeye alikuwa amemutokea mara mbili


Saulo alikufa kwa sababu ya kutokuwa mwaminifu; hakukuwa mwaminifu maana hakutii neno la Yawe na alikwenda kwa mwaguzi kumwomba shauri,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite