Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 13:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wengine walivuka muto Yordani mpaka katika inchi ya Gadi na inchi ya Gileadi. Lakini Saulo alikuwa angali kule Gilgali pamoja na watu wote waliomufuata wakitetemeka.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 13:7
15 Referans Kwoze  

Sasa uwatangazie watu wote kwamba mutu yeyote anayekuwa mwoga au anayetetemeka arudi kwake.” Basi, Gideoni akawajaribu, na watu elfu makumi mbili na mbili wakarudi kwao, akabaki na watu elfu kumi.


“Yawe atawafanya mushindwe na waadui zenu. Ninyi mutakwenda kuwashambulia kwa njia moja, lakini mutawakimbia kwa njia saba. Nanyi mutakuwa kinyaa kwa watu wote katika dunia.


Kuna mutu aliyevunjika moyo? Arudie kwake, kusudi asiwavunje wenzake moyo kama vile yeye.’


“Tulipoitwaa inchi hiyo, nikawapa makabila ya Rubeni na Gadi eneo la kuanzia upande wa kaskazini wa Aroeri karibu na Arnoni na nusu ya eneo la milima ya Gileadi, pamoja na miji yake.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


Saulo alimungojea Samweli kwa muda wa siku saba, kama vile Samweli alivyosema. Lakini Samweli hakukuja kule Gilgali na watu walianza kumwacha Saulo.


Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu nyingine ya kabila la Manase yalikuwa yamepewa inchi inayokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa, mutumishi wake.


pamoja na inchi za Gileadi, eneo la Wagesuri na Wamakati mulima wa Hermoni na inchi yote ya Basani mpaka Saleka;


Saulo pamoja na waaskari wote wa Israeli walipoyasikia maneno hayo ya Mufilistini yule, walifazaika na kuogopa sana.


Nao Waisraeli waliokuwa upande wa pili wa bonde, na wengine waliokuwa upande wa mashariki wa muto Yordani walipoona kwamba Waisraeli wamekimbia, naye Saulo na wana wake wamekufa, waliihama miji yao, wakakimbia. Wafilistini wakaenda na kukaa katika miji hiyo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite