1 Samweli 13:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
19 Wakati huo hakukuwa mufuaji yeyote wa vyuma katika inchi nzima ya Israeli, maana Wafilistini walikusudia kuwazuia Waebrania wasipate kujitengenezea mapanga au mikuki.
Alitwaa watu wote wa Yerusalemu: wakubwa wote, watu wote waliokuwa mashujaa, wafungwa elfu kumi, na wafundi wote na wafuaji wa vyuma. Hakuna aliyebaki isipokuwa wale waliokuwa wamasikini kabisa katika inchi.
Ilikuwa nyuma ya Nebukadneza mufalme wa Babeli kuwahamisha Yekonia mufalme wa Yuda mwana wa Yoyakimu, pamoja na wakubwa wa inchi ya Yuda na wafundi bora na wafuaji wa vyuma kutoka Yerusalema na kuwapeleka Babeli. Yawe akanionyesha vikapu viwili vya matunda ya tini vimewekwa mbele ya hekalu la Yawe.
Wakati huu ulikuwa nyuma ya kuondoka Yerusalema kwa mufalme Yekonia na malkia mama wa mufalme, matowashi wa mufalme, wakubwa wa inchi ya Yuda na wa Yerusalema, wafundi na wafua vyuma.