6 Samweli akawaambia: “Yawe ndiye aliyemuchagua Musa na Haruni na kuwaondoa babu zenu katika inchi ya Misri.
Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.
Haruni na Musa ndio walioambiwa na Yawe: “Mutoe watu wa Israeli kutoka inchi ya Misri, vikundi kwa vikundi.”
Alipasua jiwe maji yakabubujika; yakatiririka katika jangwa kama muto.
Musa na Haruni walikuwa makuhani wake; Samweli alikuwa kati ya waliomulilia. Walimulilia Yawe naye akawasikiliza.
Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.
Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.
Ndio haohao Musa na Haruni walioongea na mufalme wa Misri, juu ya kuwatoa Waisraeli kutoka inchi ya Misri.