Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 12:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 12:23
23 Referans Kwoze  

Kwa sababu hii hatuchoki kuwaombea ninyi, tangu siku tuliposikia habari zenu. Tunamwomba Mungu awawezeshe kujua kabisa mapenzi yake na kuwajaza hekima na akili inayotoka kwa Roho wake.


Mungu ambaye ninamwabudu kwa roho yangu yote kwa njia ya kutangaza Habari Njema ya Mwana wake, ni mushuhuda wangu kwamba ninawakumbuka siku zote


Ninamushukuru Mungu ambaye ninamutumikia kwa zamiri safi kama vile babu zangu walivyofanya, ninapokukumbuka siku zote katika maombi yangu usiku na muchana.


Usiku na muchana tunamwomba Mungu kwa bidii sana kusudi atupatie njia ya kuweza kuwaona tena na kuwaongezea kile munachokosewa katika imani yenu.


tafazali, uwasikilize kutokea kule mbinguni, usamehe zambi za watumishi wako, watu wako Waisraeli, na uwafundishe kufuata njia nzuri. Kisha unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako kwamba itakuwa mali yao.


Basi Petro akabaki akichungwa katika kifungo, lakini kanisa likaendelea kumwombea kwa Mungu pasipo kuchoka.


Hata simba wakali wanakosewa na kusikia njaa, lakini wanaomutafuta Yawe hawakosewi chochote kizuri.


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


uwasikilize kutokea kule mbinguni, na usamehe zambi za watumishi wako watu wako Waisraeli, nawe ukiwafundisha kufuata njia nzuri, unyeshe mvua katika inchi yako hii ambayo uliwapa watu wako ikuwe urizi.


Ni kwa hiyo tunamutangaza Kristo kwa watu wote. Tunaonya na kufundisha kila mutu kwa hekima yote, kusudi tuwasaidie watu wote wapate kufikia kuwa wakamilifu katika kuungana kwao na Kristo.


Munajua kwamba sikuwaficha hata neno moja lenye kuwafalia ninyi, lakini niliwahubiri na kuwafundisha katika mikutano na katika nyumba zenu.


Muhubiri alijikaza kupata maneno ya kupendeza, akaandika kwa usawa maneno ya kweli.


Nimekufundisha njia ya hekima, nimekuongoza katika njia ya usawa.


Mimi sina haki ya kujisifu kwa sababu ninatangaza Habari Njema, kwa maana nimelazimishwa kuitangaza. Basi ole kwangu kama nisipotangaza Habari Njema.


Kesho yake Musa akawaambia watu: Mumetenda zambi kubwa! Sasa nitamwendea Yawe juu kwenye mulima; labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya zambi yenu.


Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Ikiwa wao ni manabii, na ikiwa wana ujumbe kutoka kwa Yawe, basi wamusihi Yawe wa majeshi, kusudi vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yawe na katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalema, visitwaliwe na kupelekwa Babeli.


Yeremia akawajibu: Vema; nimesikia. Nitamwomba Yawe, Mungu wenu, kama mulivyonisihi; jibu lolote Yawe atakalonipa, nitawaambia; sitawaficha kitu chochote.


Lakini jambo la Waisraeli la kutaka wapewe mufalme wa kuwatawala, halikumupendeza Samweli. Naye akamwomba Yawe.


Mukuje, enyi vijana munisikilize, nami nitawafundisha kumwabudu Yawe.


Muuombee Yerusalema amani mukisema: “Wote wanaokupenda wakae katika amani!


Mukienda kwa upande wa kuume au kushoto, mutasikia sauti nyuma yenu ikisema: Njia ni hii; muifuate.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite