Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 12:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Hivyo wakamwambia Samweli: “Tafazali, utuombee sisi watumishi wako kwa Yawe, Mungu wako, kusudi tusikufe; kwa sababu tumezidisha zambi zetu kwa uovu huo wa kujitakia mufalme.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 12:19
24 Referans Kwoze  

Mumwombe Yawe maana ngurumo hii na mvua ya mawe vimezidi. Mimi nitawaacha muondoke na wala hamutabakia tena.”


Mutu akimwona ndugu yake anafanya zambi isiyoleta kifo, anapaswa kumwombea kwa Mungu, Mungu atamupa mutu yule uzima. Jambo hili linaelekea wale wanaotenda zambi isiyoleta kifo. Maana kuna zambi inayoleta kifo lakini sisemi kama ataomba juu ya hiyo.


Tena kwa upande wangu haitatokea niache kuwaombea kwa Yawe; kufanya hivyo itakuwa kumukosea Yawe. Nitaendelea kuwafundisha njia njema na ya haki.


Kwa hiyo sasa ninawasihi munisamehe zambi yangu mara hii, muniombee kwa Yawe, Mungu wenu, aniondolee kifo hiki.”


Nao wakiomba kwa imani, mugonjwa yule atapona, kwa kuwa Bwana atamurudishia afya yake. Na ikiwa amefanya zambi, atasamehewa.


Halafu Simoni akawaambia Petro na Yoane: “Muniombee ninyi wenyewe kwa Bwana, kusudi lisinipate hata neno moja kati ya maneno haya muliyosema.”


Kwa hiyo sasa enyi makuhani, mumwombe Mungu kusudi atuhurumie. Yawe wa majeshi anasema hivi: Ikiwa munamutolea matoleo ya aina hiyo, kweli atawakubali?


Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!


Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta, walikuomba musaada ulipowaazibu.


Kwa hiyo mutwae ngombe dume saba na kondoo dume saba, muende kwa mutumishi wangu Yobu, mutoe nyama wale kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Naye mutumishi wangu Yobu atawaombea, nami nitaisikiliza maombi yake na kuacha kuwatendea kulingana na upumbafu wenu; maana hamukusema ukweli juu yangu kama mutumishi wangu Yobu alivyofanya.”


Basi, wakamwambia Samweli: “Usiache kumulilia Yawe, Mungu wetu, kwa ajili yetu. Endelea kumulilia atuokoe kutokana na Wafilistini.”


Kisha, Samweli akawaita Waisraeli wote wakutane kule Misipa, akawaambia: “Kule nitamwomba Yawe kwa ajili yenu.”


Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”


Basi, watu wakamwendea Musa, wakamwambia: Tumetenda zambi kwa kumunungunikia Yawe na wewe vilevile. Umwombe Yawe atuondolee nyoka hawa. Kwa hiyo, Musa akawaombea watu.


Sasa, mufalme muliyejichagulia ndiye huyu hapa. Mulimwomba Yawe awape mufalme, naye amewapa.


Sasa si wakati wa kuvuna ngano? Lakini mimi nitamwomba Yawe alete radi na mvua, nanyi mutatambua na kuona kwamba uovu wenu muliotenda mbele ya Yawe kwa kujitakia mufalme, ni mukubwa.”


Samweli akawajibu: “Musiogope. Ingawa mumefanya uovu huu, musiache kumufuata Yawe, lakini mumutumikie kwa moyo wenu wote.


Mungu anatimiza mapenzi yake katika dunia, ikuwe ni kwa ajili ya kuwaazibu watu, au kwa ajili ya kuonyesha wema wake.


Ikiwa wao ni manabii, na ikiwa wana ujumbe kutoka kwa Yawe, basi wamusihi Yawe wa majeshi, kusudi vyombo vilivyobaki katika nyumba ya Yawe na katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalema, visitwaliwe na kupelekwa Babeli.


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Kesho yake Musa akawaambia watu: Mumetenda zambi kubwa! Sasa nitamwendea Yawe juu kwenye mulima; labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya zambi yenu.


Lakini jambo la Waisraeli la kutaka wapewe mufalme wa kuwatawala, halikumupendeza Samweli. Naye akamwomba Yawe.


Mufalme Zedekia aliwatuma Yehukali mwana wa Selemia, pamoja na kuhani Zefania mwana wa Maseya, kwa nabii Yeremia kusema awaombee kwa Yawe, Mungu wao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite