Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 12:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini mulipomwona mufalme Nahasi wa Waamoni amekuja kuwashambulia, mukamukataa Yawe ambaye ndiye Mufalme wenu, mukaniambia: ‘Hapana! Mufalme ndiye atakayetutawala’.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 12:12
15 Referans Kwoze  

Gideoni akawajibu: “Mimi sitakuwa mutawala wenu wala mwana wangu hatakuwa mutawala wenu. Yawe ndiye atakayekuwa mutawala wenu.”


Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”


Yuko wapi sasa mufalme wenu awaokoe? Wako wapi wale wakubwa wenu wawalinde? Ninyi ndio mulioomba: Utupatie mufalme na wakubwa watutawale.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Hata hivyo wewe Mungu ni mufalme wetu tangu zamani; umefanya mambo makubwa ya kuokoa katika inchi.


Lakini watoto hao hawakufuata mwenendo wa baba yao. Lakini walianza kujitafutia faida. Wakapokea kituliro na kupotosha haki.


Lakini leo mumeishambulia jamaa ya baba yangu na kuwaua wana makumi saba juu ya jiwe moja, halafu mumemufanya Abimeleki mutoto wa mujakazi wa baba, akuwe mufalme wa wakaaji wa Sekemu kwa sababu tu ni mutu wa ukoo wenu.


Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.


“Nitasimamisha agano langu nawe, wazao wako na vizazi vyao vyote milele; nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazao wako milele.


Vilevile Wayuda waliokuwa katika inchi ya Moabu na kati ya Waamoni na katika inchi ya Edomu na inchi zingine, waliposikia kwamba mufalme wa Babeli amewaruhusu Wayuda wengine kubaki katika inchi ya Yuda na kwamba amemusimika Gedalia mwana wa Ahikamu, mujukuu wa Safanu kuwa mutawala wao,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite