Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 12:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Babu zenu wakamulilia Yawe, wakisema: ‘Tumefanya zambi kwa sababu tumekuacha wewe Yawe, kwa kutumikia sanamu za mungu Bali na Astaroti. Utuokoe kutoka katika mikono ya waadui zetu, nasi tutakutumikia’.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 12:10
18 Referans Kwoze  

Basi wakamulilia Yawe, wakisema: “Tumetenda zambi mbele yako, maana tumekuacha wewe Mungu wetu, tukatumikia Mabali.”


Walimwacha Yawe, wakatumikia Mabali na Mastaroti.


Waisraeli wakamulilia Yawe, naye akawapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Otinieli mwana wa Kenazi, ndugu mudogo wa Kalebu.


Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe. Wakamusahau Yawe, Mungu wao, wakaabudu Mabali na Maashera.


Maana Yawe ni mwamuzi wetu, yeye ni mutawala wetu; Yawe ni mufalme wetu, yeye ndiye anayetuokoa.


Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta, walikuomba musaada ulipowaazibu.


Hata hivyo Mungu aliona taabu yao, wakati aliposikia kilio chao;


Tangu Sanduku la Yawe lilipopelekwa katika muji wa Kiriati-Yearimu, kulipita muda murefu, miaka makumi mbili hivi. Wakati huo Waisraeli wote walimulilia Yawe.


Waisraeli walipomulilia Yawe awaondolee taabu walizopata kwa Wamidiani,


Mufalme Asikie alikuwa na magari ya vita mia tisa ya chuma. Aliwagandamiza sana Waisraeli kwa miaka makumi mbili; nao wakamulilia Yawe awasaidie.


Lakini Waisraeli walipomulilia Yawe, basi, aliwapelekea mutu wa kuwakomboa, ni kusema Ehudu, mwana wa Gera wa kabila la Benjamina. Alikuwa mwenye kutumikisha zaidi mukono wa kushoto. Waisraeli wakamutuma apeleke zawadi zao kwa Mwana-Ngombe, mufalme wa Moabu.


nusu ya Gileadi, Astaroti, Edirei, ambayo ilikuwa ya mufalme Ogi wa Basani. Nusu ya wazao wa Makiri mwana wa Manase, eneo hili walipewa kulingana na ukoo zao.


Basi, Waisraeli walitenda uovu mbele ya Yawe na kuabudu Mabali.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika kule Misipa. Walichota maji na kuyamimina mbele ya Yawe, wakafunga kula chakula siku ile yote na kusema: “Tumetenda zambi mbele ya Yawe.” Samweli akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kule Misipa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite