Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 10:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini leo hii mumenikataa mimi Mungu wenu ambaye ninawaokoa kutoka hasara na huzuni zenu, nanyi mumesema: ‘Hapana! Utuwekee mufalme juu yetu.’ Sasa basi, mujikusanye wote mbele yangu mukiwa katika makabila yenu na kwa maelfu yenu.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 10:19
18 Referans Kwoze  

Lakini mulipomwona mufalme Nahasi wa Waamoni amekuja kuwashambulia, mukamukataa Yawe ambaye ndiye Mufalme wenu, mukaniambia: ‘Hapana! Mufalme ndiye atakayetutawala’.


Hata hivyo watu walikataa kumusikiliza Samweli, wakasema: “Hapana! Sisi tutakuwa na mufalme juu yetu,


Kisha Yoshua akayakusanya makabila yote ya Waisraeli kule Sekemu. Akawaita wazee, viongozi, waamuzi na wakubwa wa Waisraeli, nao wakakuja mbele ya Mungu.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Umwambie Eleazari mwana wa kuhani Haruni atoe hivyo vyetezo kwenye moto, atupe mbali moto unaokuwa ndani, maana vyetezo hivyo ni vitakatifu.


lakini kwa muda wa mwezi muzima! Mutaikula mpaka iwatoke ndani ya pua, mpaka muichukie. Yote hayo ni kwa sababu mumemukataa Yawe anayekuwa hapahapa kati yenu, na kulia mbele yake mukisema: Kwa nini tulitoka Misri?


“Mutakapokwisha kuingia katika inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa, mukirizi na kukaa humo, nanyi mukisema kwamba mutaweka mufalme juu yenu, kama vile mataifa yote yanayowazunguka,


Gideoni akawajibu: “Mimi sitakuwa mutawala wenu wala mwana wangu hatakuwa mutawala wenu. Yawe ndiye atakayekuwa mutawala wenu.”


Kisha Samweli akayapanga makabila yote ya Waisraeli, kabila la Benjamina likaangukiwa na kura.


Hivyo Yawe aliwapa Waisraeli ushindi. Vita ilienea mpaka kupita Beti-Aweni.


Saulo akasema: “Mukuje hapa enyi viongozi wa watu, tujue ni zambi gani tumetenda leo.


Kura inapigwa kwa kujua yatakayotukia, lakini uamuzi ni wa Yawe.


Yawe alizidi kujionyesha kule Shilo, ambako alimutokea Samweli na kuongea naye. Naye Samweli aliposema kitu, Waisraeli wote walimusikiliza.


Wakati huo, Wafilistini walikutana pamoja, wapigane na Waisraeli. Waisraeli walipiga kambi yao kule Ebeni-Ezeri, na Wafilistini wakapiga kambi yao kule Afeki.


wakamwambia: “Angalia, wewe sasa ni muzee na watoto wako hawafuati mwenendo wako. Hivyo, utuchagulie mufalme wa kututawala sawa vile inavyokuwa kwa mataifa mengine.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite