17 Samweli aliwaita watu wote wakusanyike mbele ya Yawe kule Misipa.
Watu wote wa Israeli, kutokea Dani mpaka Beri-Seba, pamoja na watu wa inchi ya Gileadi, wakakusanyika kule Misipa, mbele ya Yawe.
Yefuta akafuatana na wazee wa Gileadi, nao watu wakamufanya kiongozi wao. Yefuta akasema masharti yake kule Misipa mbele ya Yawe.
Watu wote wakaenda Gilgali, na walipofika kule, wakamusimika Saulo kuwa mufalme mbele ya Yawe. Wakamutolea Yawe sadaka za amani pale. Na Saulo pamoja na watu wote wa Israeli wakafurahi sana.
Kwa hasira yangu mimi nikawapa mufalme, kisha nikamwondoa kwa kasirani yangu.
Kila mwaka Samweli alitembelea Beteli, Gilgali na Misipa, na kuwaamulia Waisraeli haki zao katika miji hiyo yote.