Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Elekana alimupa Hana fungu kubwa la nyama ya sadaka kwa sababu alimupenda sana ingawa Yawe hakumujalia watoto.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 1:5
9 Referans Kwoze  

Yakobo akamukasirikia Rakeli na kumwambia: “Mimi nimekuwa pahali pa Mungu aliyekuzuia kupata watoto?”


Aliwapa kila mumoja wao nguo za kubadilisha, lakini akamupa Benjamina vikoroti mia tatu vya feza na nguo tano za kubadilisha.


Hapo mbele Yawe alikuwa amewazuia wanawake wote wa nyumba ya Abimeleki kupata watoto kwa sababu ya Sara, muke wa Abrahamu.


Basi, Sarai, muke wa Abramu, alikuwa bado hajamuzalia mutoto, naye alikuwa na mujakazi aliyeitwa Hagari, kutoka Misri.


Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.


“Ikiwa mwanaume fulani ana wake wawili naye anamupenda mumoja kuliko mwingine, nao wanawake hao wamemuzalia watoto wanaume, na mutoto wa kwanza kuzaliwa ni wa yule mama asiyemupenda,


Rakeli alipoona kwamba hajamuzalia Yakobo watoto, alimwonea Lea dada yake wivu, akamwambia Yakobo: “Unipatie watoto, kama sivyo, nitakufa.”


Sarai hakukuwa na mutoto kwa sababu alikuwa tasa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite