Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 1:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Mume wake Elekana, akamujibu: “Fanya unaloona linafaa. Ngojea mpaka utakapomwachisha mutoto kunyonya. Yawe afanye kiapo chako kuwa kweli.” Basi, Hana alibaki kwake, akaendelea kumulea mutoto wake mpaka alipomwachisha kunyonya.

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 1:23
12 Referans Kwoze  

Basi, sasa, ee Yawe Mungu, uikamilishe ile ahadi uliyosema juu yangu mimi mutumishi wako na juu ya jamaa yangu.


Yesu alipokuwa akisema maneno hayo, mwanamuke mumoja kati ya kundi la watu akasema kwa sauti kubwa: “Heri mwanamuke yule aliyekuzaa na kukunyonyesha!”


Wanawake wenye mimba na wenye kunyonyesha watapata hasara katika siku zile!


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Wanasema: “Alimutegemea Yawe, basi, Mungu amuponyeshe! Kama Mungu anapendezwa naye, basi, amwokoe!”


Halafu Eli akamwambia: “Kwenda kwa amani; naye Mungu wa Israeli akupe kile ulichomwomba.”


kisha mume wake akisikia jambo hilo naye hamupingi, wala kumwambia kitu, basi, viapo vyake vyote vitamufunga; vilevile na ahadi zake zote zitamufunga.


Kisha Saulo akawaambia watu: “Twende tuwafuatilie Wafilistini usiku, tuwashambulie na kunyanganya mali zao mpaka asubui. Hatutamwacha mutu yeyote muzima.” Watu wakamwambia: “Fanya unachoona kuwa chema kwako.” Lakini kuhani akawaambia: “Kwanza tuombe shauri kwa Yawe.”


Kwa hiyo, Saulo akawaambia: “Ninyi wote musimame upande ule, halafu mimi na mwana wangu Yonatani tutasimama upande huu.” Wao wakajibu: “Fanya chochote unachoona kinafaa.”


Nilipoamuka asubui na kutaka kumunyonyesha mwana wangu, nikakuta mutoto amekufa. Nilipochunguza sana, nikagundua kwamba hakukuwa mwana wangu niliyemuzaa.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite