Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 1:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Lakini mara hii Hana hakuenda, maana alimwambia mume wake hivi: “Mara tu mutoto atakapoachishwa kunyonya, nitamupeleka kusudi awekwe mbele ya Yawe, abakie kule siku zote.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 1:22
17 Referans Kwoze  

Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”


Siku zilipotimia za Maria na Yosefu kutakaswa kama vile Sheria ya Musa inavyoagiza, wakamupeleka mutoto Yerusalema, kusudi wapate kumutolea kwa Bwana.


Wakati huo, kijana Samweli alipokuwa anamutumikia Yawe chini ya uangalizi wa Eli, ujumbe kutoka kwa Yawe ulikuwa mara haba tu; hata na maono kutoka kwake yalipatikana mara chache.


Wakati ule, kijana Samweli aliendelea kumutumikia Yawe, akiwa amevaa kizibao cha kitani.


Kisha, Elekana akarudi kwake Rama. Lakini mutoto Samweli akabaki Shilo kwa kumutumikia Yawe chini ya uongozi wa kuhani Eli.


“Wanaume wote wa taifa lenu watakuja mbele ya Yawe, Mungu wenu, mara tatu kila mwaka, pahali ambapo Yawe, Mungu wenu atachagua: wakati wa sikukuu ya Pasaka, sikukuu ya kuvuna na wakati wa sikukuu ya vibanda. Wasitokee mbele ya Yawe mikono mitupu.


Musiuzishe mashamba kabisa, maana hiyo ni mali yangu na ninyi ni wageni na wasafiri katika inchi yangu.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”


Jambo moja nimemwomba Yawe, ninatafuta hili tu: nikae ndani ya nyumba ya Yawe siku zote za maisha yangu, niuone uzuri wa Yawe, na kutafuta maongozi yake ndani ya hekalu lake.


Kweli, uzuri na wema wako vitakuwa pamoja nami siku zote za maisha yangu; nami nitakaa katika nyumba ya Yawe milele.


Ninyi mutawaambia: ‘Sanduku la Agano la Yawe lilipopitishwa katika muto Yordani, maji ya muto huo yalizuiliwa yasitiririke!’ Kwa hiyo mawe haya yatakuwa ukumbusho kwa Waisraeli milele.”


basi, bwana wake atamuleta mbele ya Mungu. Kisha atamupeleka kwenye mulango au kwenye kizingiti na kumutoboa sikio lake kwa chuma chenye kuchongwa. Naye atamutumikia bwana wake maisha yake yote.


Samweli akamujibu Saulo: “Umefanya kipumbafu. Haukutii mambo Yawe, Mungu wako, aliyokuamuru. Kama ungetii, Yawe angeudumisha milele ufalme wako juu ya Israeli.


Daudi akamujibu Akisi: “Kweli! Utaona kitu ambacho mutumishi wako anaweza kufanya.” Akisi akamwambia: “Nami nitakufanya kuwa mulinzi wangu wa pekee wa maisha.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite