Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




1 Samweli 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Akafanya kiapo akisema: “Ee Yawe wa majeshi, kama tu utayaangalia mateso yangu mimi mujakazi wako, ukinikumbuka mimi, bila kunisahau, mimi mujakazi wako, ukinijalia mimi mujakazi wako mutoto mwanaume, nitakupa wewe Yawe mutoto huyo akuwe wako maisha yake yote; wembe hautapita kwenye kichwa chake hata kidogo.”

Gade chapit la Kopi




1 Samweli 1:11
25 Referans Kwoze  

kwa maana utabeba mimba na kuzaa mutoto mwanaume. Nywele za mutoto huyo zisinyolewe hata kidogo, maana atakuwa Munaziri wa Mungu tangu kuzaliwa kwake. Naye ataanza kuwakomboa Waisraeli toka katika mikono ya Wafilistini.”


Siku zote za kiapo chake cha kujitenga, hatanyoa nywele zake. Mpaka muda wa kiapo chake cha kujitakasa kwa Yawe utakapomalizika, atakuwa mutakatifu, ataacha nywele zake zikuwe ndefu.


Ni afazali usifanye ahadi kuliko kufanya ahadi kisha usiitimize.


Lea akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Rubeni, akisema: “Yawe ameona mateso yangu; bila shaka sasa mume wangu atanipenda.”


Uangalie mateso yangu na taabu yangu; unisamehe zambi zangu zote.


Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.


Kisha Mungu akamukumbuka Rakeli, akakubali ombi lake na kumujalia kupata watoto.


Yefuta akamwapia Yawe akisema: “Kama utawatia Waamoni katika mikono yangu,


Muda wote atakaokuwa munaziri atakuwa mutakatifu kwa Yawe.


Kisha Yakobo akafanya kiapo akisema: “Ikiwa, ee Mungu, utakuwa pamoja nami na kunilinda katika safari yangu, ukinipa chakula na nguo


Labda Yawe ataangalia mateso yangu, naye atanilipa wema kwa laana hii ninayopata leo.”


Hapo, Waisraeli wakamwekea Yawe kiapo wakisema: Kama ukiwatia watu hawa katika mikono yetu, basi tutaangamiza kabisa miji yao.


Kuhani atamutoa mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, naye atamufanyia ibada ya upatanisho, kwa sababu alitenda zambi kwa sababu ya maiti. Siku hiyohiyo atatakasa kichwa chake


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Kisha Mungu akamukumbuka Noa na nyama wote wa pori na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya inchi, maji yakaanza kupunguka.


Hana alikuwa na huzuni sana. Na alipokuwa anamwomba Yawe akakuwa analia kwa uchungu.


Hana aliendelea kumwomba Yawe kwa muda murefu, na kuhani Eli akakuwa anaangalia midomo yake.


Lakini mara hii Hana hakuenda, maana alimwambia mume wake hivi: “Mara tu mutoto atakapoachishwa kunyonya, nitamupeleka kusudi awekwe mbele ya Yawe, abakie kule siku zote.”


Nilimwomba anipe mutoto huyu, na yeye alinipa kile nilichomwomba.


Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


Eli aliwabariki Elekana na muke wake, akisema: “Yawe akupe wewe Elekana watoto wengine kwa mwanamuke huyu kusudi wakamate nafasi ya yule uliyemupa Yawe.” Kisha wao walirudi kwao.


Nikuambie nini mwana wangu? Nikuambie nini mwana wangu niliyezaa? Nikuambie nini wewe niliyeomba kwa Mungu?


Uwaambie Waisraeli hivi: Mutu akifanya kiapo cha kumutolea Yawe mwanadamu, mutu huyu anaweza kuondoa kiapo chake kwa kulipa kipimo cha feza kinachokadiriwa kama hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite