Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Yuda 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mukumbuke vilevile watu wa Sodoma na Gomora na wa miji iliyokuwa kandokando wanaokuwa sawasawa na wamalaika hawa. Walifanya uasherati na mambo ya kimwili yasiyokuwa ya kawaida ya asili. Watu hawa wanapokea hukumu ya moto wa milele kuwa mufano wazi kwa watu wote.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Yuda 1:7
27 Iomraidhean Croise  

Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Basi, Yawe akasema: “Kuna malalamiko mengi juu ya watu wa Sodoma na Gomora, na zambi yao ni kubwa sana.


Wakamwita Loti na kumwuliza: “Wako wapi wale wanaume waliokuja kwako? Uwatoshe inje. Tunataka kulala nao.”


Matendo mengine ya Yosafati, ushujaa wake na vita alivyopigana, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda.


Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.


Babeli ni utukufu wa falme zote na sifa na majivuno ya Wakaldea utakuwa kama Sodoma na Gomora, wakati Mungu alipoiangamiza.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Mutu huyo akuwe kama miji Yawe aliyoiangusha bila huruma. Mutu huyo asikie kilio asubui, na muchana asikie kelele za vita,


Kama vile mimi Yawe nilivyoiangamiza miji ya Sodoma na Gomora na miji ya jirani, vilevile hakutakuwa mutu yeyote atakayeishi humo. Kweli, hakuna mutu yeyote atakeyekaa huko. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kosa la watu wangu lilikuwa kubwa kuliko zambi za watu wa Sodoma, muji ambao uliteketezwa kwa rafla bila kuwa na muda wa kunyoosha mukono.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Wale waliobaki kati yenu, walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kweli ninawaambia: kwa Siku ya hukumu, watu wa muji ule wataazibiwa vikali zaidi kuliko watu wa muji wa Sodoma na wa Gomora.


Kwa hiyo ninawaambia kwamba kwa Siku ya hukumu, wewe utaazibiwa zaidi kuliko watu wa Sodoma!”


“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!


Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikashuka kama mvua toka mbinguni na kuwaangamiza wote.


Ninyi munajua hakika kwamba watenda mabaya hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu. Musidanganyike: waasherati, wenye kuabudu sanamu, wazinzi, waasherati wa muke kwa muke na mume kwa mume,


Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’


na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,


katikati ya ndimi za moto kwa kuazibu wale wanaokataa kumujua Mungu na wale wasiokubali Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.


Watu wengi watafuata matendo yao maovu na kwa ajili yao, mafundisho ya Bwana yatazarauliwa.


Vilevile Mungu alihukumu muji wa Sodoma na Gomora na kuiteketeza kwa moto. Kwa njia hiyo, alionyesha mufano wa mambo yatakayotokea kwa watu waovu.


Lakini kwa nguvu ya neno lile lile, mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa kuteketezwa kwa moto. Zinalindwa kwa ajili ya Siku ile ambayo watu wabaya watahukumiwa na kuangamizwa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan