Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Yoeli 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Halafu, watu wote watakaoomba kwa jina la Yawe wataokolewa. Katika mulima Sayuni na Yerusalema, kutakuwa watu watakaoponyoka, kama vile Yawe alivyosema: wale aliowachagua watabaki wazima.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Yoeli 3:5
15 Iomraidhean Croise  

Wakati huo Hazaeli mufalme wa Aramu akaushambulia muji wa Gati na kuuteka. Lakini Hazaeli alipoelekea Yerusalema kusudi aushambulie,


Ahazi akatwaa feza na zahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yawe na hazina iliyokuwa katika nyumba ya mufalme na kumupelekea kama zawadi mufalme wa Asuria.


Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Kwa hiyo, siku zinakuja siku ambapo watu hawataapa tena, wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa watu wa Israeli kutoka katika inchi ya Misri.


Sikiliza! Wakimbizi na wenye kutoroka kutoka inchi ya Babeli wanakuja kutangaza huko Sayuni jinsi Yawe, Mungu wetu, alivyolipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake.


Yawe amezichochea roho za wafalme wa Wamedi, kwa maana amekusudia kuiangamiza Babeli. Kweli, hicho ndicho kisasi cha Yawe; analipiza kisasi kwa ajili ya hekalu lake. Munoe mishale yenu! Mutwae ngao!


Kwa hiyo, toa unabii, uwaambie kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Enyi watu wangu, nitayafunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu. Nitawarudisha ndani ya nyumba zenu katika inchi ya Israeli.


Pahali pa miungu hiyo atamuheshimu mungu mulinzi wa kuta za muji, ambaye babu zake hawakumwabudu hata kidogo. Atamutolea zahabu, feza na mawe ya bei kali, na zawadi za bei kubwa.


Lakini wale waliobaki watakaa kwa mulima Sayuni nao utakuwa mulima mutakatifu. Wazao wa Yakobo watanyanganya inchi yao toka kwa wale waliokuwa wameinyanganya.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan