Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Wafilipi 4:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Muonyeshe upole wenu kwa watu wote, kwa maana Bwana yuko karibu kurudia.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Wafilipi 4:5
25 Iomraidhean Croise  

“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Basi musijisumbue kwa ajili ya kesho, kwa maana kesho itajisumbukia yenyewe. Kila siku ina masumbuko yake inayoitoshelea.


“Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla


Kama mutu hamupendi Bwana, alaaniwe! Bwana wetu, kuja!


Kweli mambo haya ya kuwa na mashitaki kati yenu yanahakikisha kwamba mumeshindwa kabisa. Si ingekuwa vizuri zaidi kwenu kuvumilia ubaya? Si ingekuwa vizuri zaidi kunyanganywa mali zenu?


Kwa hiyo chakula kikimwangusha ndugu yangu katika zambi, nitajizuiza kula nyama siku zote kusudi nisimwangushe ndugu yangu.


Na kila mutu anayefanya mashindano katika michezo anajizuiza na vitu vingi katika mazoezi yake. Basi wanafanya hivi kusudi wapate taji yenye kuharibika; lakini sisi tunafanya vile, kusudi tupate taji isiyoharibika.


Sasa mimi Paulo mwenyewe ninawaomba kwa upole na kwa wema sawa na ule wa Kristo; mimi yule ambaye wanasema juu yake kwamba ni mupole wakati ninapokuwa pamoja nanyi, lakini ni mukali wakati ninapokuwa mbali nanyi.


musifazaike upesi wala kuogopa kwamba Siku ya kurudi kwa Bwana imekwisha kutimia. Inawezekana munafahamu mambo yale kwa njia ya unabii, mahubiri na barua inayosemeka kwamba imetoka kwetu.


Uwaambie wasiseme mabaya juu ya mutu, lakini wakuwe wenye kupenda amani na wema, na wenye kuonyesha upole mbele ya kila mutu.


Tusiache kukusanyika pamoja, kama vile wamoja wanavyozoea kufanya. Lakini tuonyane, na zaidi sana kufuatana na vile munavyoona kwamba Siku ya Bwana inakaribia.


Kwa maana, kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema: “Kunabaki wakati kidogo sana, yule anayepaswa kuja, afike wala hatakawia.


Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao alitangulia kushuhudia mateso yatakayomupata Kristo na utukufu utakaokuwa nyuma. Nao walijitolea kusudi wapate kuvumbua wakati gani na kwa njia gani mambo haya yatafanyika.


Mwisho wa vitu vyote unakaribia kutimia. Kwa hiyo mukuwe wenye akili na waangalifu, kusudi mukuwe na uwezo wa kuomba.


Mwenye kushuhudia maneno hayo anasema: “Ndiyo, ninakuja upesi!” Amina! Kuja Ee Bwana Yesu!


Yesu anasema: “Sikiliza, ninakuja upesi! Heri yule anayeshika maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki!”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan