Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Wafilipi 4:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kwa hiyo wandugu zangu wapendwa, niko na hamu sana ya kuwaona tena. Ninyi ndio munaokuwa furaha yangu na zawadi ya ushindi nitakayopokea. Ninyi wapendwa wangu, ninawaomba musimame imara katika ushirika wenu na Bwana.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Wafilipi 4:1
35 Iomraidhean Croise  

Ningeyabeba kwa sifa juu ya mabega yangu na kuyavaa kwenye kichwa kama taji.


Wimbo wa safari za kidini. Wanaomutegemea Yawe, wako kama mulima Sayuni, ambao hautikisiki lakini unabaki imara siku zote.


Umutegemee Yawe! Ujitie moyo, ukuwe hodari! Umutegemee Yawe!


Na watu wote watawachukia kwa ajili yangu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Basi Yesu akawaambia wale Wayuda waliomwamini: “Kama mukitii mafundisho yangu, ninyi ni wanafunzi wangu hakika.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Nao walikuwa wakijitoa kufuata mafundisho ya mitume, kuishi katika ushirika wa kindugu, kumega mukate na kuomba.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Basi wandugu zangu wapenzi, musimame imara bila kutikisika. Muendelee kumutumikia Bwana siku zote, mukijua kwamba masumbuko munayopata kwa ajili ya Bwana hayatapita bure.


Mukeshe, musimame imara katika imani, mukuwe hodari na wenye nguvu.


maana munayafahamu sasa kwa sehemu tu. Kwa Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu mutaweza kujivuna kwa ajili yetu kama vile tutakavyojivuna kwa ajili yenu.


Kristo ametukomboa katika utumwa kusudi tukuwe huru kabisa. Basi, musimame imara wala musijitie tena katika vifungo vya utumwa.


Kitu cha lazima ni kwamba mukuwe na mwenendo unaolingana na mafundisho ya Habari Njema ya Kristo. Kwa hivi hata kama nikikuja kuwaona au hata kama nisipokuja, nipate tu kusikia kwamba munasimama imara katika nia moja, na kwamba wote pamoja munapigana vita kwa ajili ya imani inayotokana na Habari Njema.


Mungu ni mushuhuda wangu kwamba ninawapenda sana ninyi wote na moyo wa upendo mukubwa wa Yesu Kristo.


mukiwatangazia habari inayoleta uzima. Hivi nitapata sababu ya kujivuna Siku ile ya kurudia kwa Kristo kwa maana itakuwa kitambulisho cha kuhakikisha kwamba bidii yangu na kazi yangu havikupotea bure.


Yeye yuko na hamu sana kuwaona ninyi wote, naye anahuzunika sana kwa sababu mulisikia kwamba alikuwa mugonjwa.


Mwanainchi mwenzenu Epafra anawasalimia vilevile. Yeye ni mutumishi wa Yesu Kristo, hachoki kwa kuwaombea ninyi, kusudi musimame imara mukikomaa kiroho na kuwa tayari kwa kutimiza kabisa mapenzi ya Mungu.


Vilevile aitie mioyo yenu nguvu nanyi mutapata kuwa watakatifu na bila kosa mbele ya Mungu Baba yetu siku Bwana wetu Yesu atakaporudia pamoja na watakatifu wake wote.


Basi wandugu, musimame imara na mushike mafundisho yetu tuliyowatolea, ikiwa kwa mahubiri au kwa barua yetu.


Basi wewe mwana wangu, ukuwe hodari kwa njia ya neema uliyopata katika kuungana kwako na Kristo Yesu.


Tuendelee kuchunga lile tumaini tuliloshuhudia bila kuchoka, kwa maana Mungu aliyetupatia ahadi ni mwaminifu.


Kwa maana sisi wote tunaishi katika ushirika na Kristo ikiwa tunachunga mpaka mwisho lile tumaini tulilopata kwa mwanzo.


Basi, kwa kuwa tuko na Kuhani Mukubwa zaidi aliyeingia mbinguni, ndiye Yesu Mwana wa Mungu, tushikamane sana na imani tunayotangaza.


Basi ninyi wapendwa wangu, mumekwisha kutambua mambo haya. Mujiangalie vizuri kusudi musipotoshwe na makosa ya watu waovu na kukosa kusimama imara.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan