Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Wafilipi 3:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Sisi ndio wenye kutahiriwa kwa kweli, maana tunamwabudu Mungu kwa uongozi wa Roho wake na kujivuna kwa ajili ya Yesu Kristo. Sisi hatuweki tumaini letu katika mambo ya kimwili.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Wafilipi 3:3
32 Iomraidhean Croise  

Mujisifu kwa ajili ya jina lake takatifu; wanaomutafuta Yawe wafurahi.


Lakini wazao wa Israeli watapata ushindi toka kwa Yawe na kufurahi.


Enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema, mujitahiri, mukiondoa govi za mioyo yenu, mupate kujitoa kwa Yawe. Kama si vile, kasirani yangu itawaka kama moto, nayo itaunguza wala hakuna atakayeizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Mungu ambaye ninamwabudu kwa roho yangu yote kwa njia ya kutangaza Habari Njema ya Mwana wake, ni mushuhuda wangu kwamba ninawakumbuka siku zote


Basi katika kuungana kwangu na Kristo, ninaweza kujisifu kwa ajili ya kazi hii ninayomutumikia Mungu.


Lakini sasa tumekuwa huru toka vifungo vya Sheria, kwa maana tunakuwa kama waliokufa kufuatana na mambo yale yaliyotufunga. Kwa hiyo tunaweza kumutumikia Mungu kwa kufuata njia mupya chini ya uongozi wa Roho wake, wala si kufuata njia ya zamani chini ya uongozi wa maandiko ya Sheria.


Kwa maana hamukupewa roho anayewafanya muishi katika utumwa na kuwatia tena woga, lakini mulipewa Roho anayewafanya mukubaliwe kuwa watoto wa Mungu. Na kwa uwezo wa Roho huyo, tunaweza kumwita Mungu “Baba.”


wala nguvu za juu, wala nguvu za chini, wala kiumbe kingine chochote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu aliouonyesha kwetu kwa njia ya Kristo Yesu Bwana wetu.


Sisemi kwamba ahadi ya Mungu haikutimia. Kwa maana si wote wanaotoka katika uzao wa Israeli ndio Waisraeli wa kweli,


Watu wengi wanajivuna kwa namna ya kimwili, kwa sababu hiyo mimi nitajivuna vilevile.


Kufuatana na vile tunavyoishi kwa nguvu za Roho, basi tufuate maongozi ya Roho vilevile.


Na wote wanaofuata kanuni hii katika maisha yao pamoja na watu wa Mungu wanaohesabiwa kama Waisraeli wa kweli, ninawatakia amani na wema.


Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.


Yawe, Mungu wenu, atawafanya ninyi na wazao wenu mukuwe na moyo wa utii kusudi mumupende yeye kwa moyo wenu wote na roho yenu, mupate kuishi.


Barua hii inatoka kwangu mimi Paulo na kwa ndugu yetu Timoteo, sisi watumishi wa Yesu Kristo. Tunawaandikia watu wote wa Mungu wanaoungana na Yesu Kristo, wanaoishi Filipi, pamoja na wazee wa kanisa na wasaidizi.


Sitaki kusema kwamba nimekwisha kufikia mwisho au kwamba nimekwisha kuwa mukamilifu. Lakini ninakaza mwendo kusudi nipate kushinda na kupokea zawadi, kwa maana Yesu Kristo amekwisha kunipokea nikuwe wake.


Kwa hiyo ninakaza mwendo mpaka mwisho nipate kupokea ile zawadi Mungu aliyotuitia katika mbingu kwa njia ya Yesu Kristo.


Katika kuungana naye, mumetahiriwa wala si kwa mikono ya watu, lakini mumetahiriwa na Kristo, na kutahiriwa kule kumewakomboa toka katika hali zaifu ya kimwili.


Lakini ninyi wapendwa wangu, muendelee kusimama imara katika imani yenu inayokuwa takatifu sana, mukiomba kwa uwezo wa Roho Mutakatifu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan