Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Wafilipi 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Musifanye jambo lolote kwa roho ya mapingano wala kwa kujivuna bure, lakini munyenyekeane kila mutu akimuhesabu mwenzake kuwa muzuri kuliko yeye mwenyewe.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Wafilipi 2:3
24 Iomraidhean Croise  

Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.


Yesu akaongeza kusema: “Ninawaambia kwamba mutu huyu alirudia kwake akiwa amehesabiwa kuwa na haki mbele ya Mungu, lakini si yule Mufarisayo. Kwa maana kila mutu anayejiinua atashushwa, lakini anayejishusha atainuliwa.”


Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.


Tukuwe na mwenendo muzuri unaostahili wakati wa muchana, tukijilinda na ulafi na ulevi, uasherati na uzinzi, magombano na wivu.


Lakini wapingaji na wale wanaokataa kufuata ukweli, wakifuata uovu, wataangukiwa na kasirani na hasira ya Mungu.


Kwa maana mimi ni mudogo kati ya mitume wote, nami sistahili hata kuitwa mutume, kwa maana nilitesa kanisa la Mungu.


kwa sababu mungali munatawaliwa na mambo ya kidunia. Kwa maana ikiwa kungali wivu na ugomvi katikati yenu, haionyeshi kwamba munatawaliwa na mambo ya kidunia, nanyi munaishi kufuatana na hali ya kimutu?


Kwa maana ninaogopa kwamba wakati ninapokuja kwenu, sitawakuta sawa vile ninavyotaka, nanyi hamutanikuta sawa vile munavyotaka. Ninaogopa kuwakuta katika fitina, wivu, kasirani, ugomvi, masingiziano, matetano, majivuno na fujo.


Lakini kama mukiumana na kukulana kama nyama wa pori, muangalie vizuri musiteketezane.


Tusijivune, tusichokozane wala kuoneana wivu.


Mukuwe wanyenyekevu kabisa, wapole na wavumilivu. Muvumiliane ninyi kwa ninyi kwa upendo.


Mukuwe na utii ninyi kwa ninyi kwa kumuheshimu Kristo.


Mufanye kila kitu bila manunguniko wala mabishano,


Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.


Lakini sasa mutupilie mbali mambo haya yote: kasirani, chuki, uovu, masingiziano na musiseme neno lolote baya.


yeye anajaa majivuno wala hajui kitu. Yeye yuko na ulema wa kubishana na kugombezana juu ya maana ya maneno. Na hayo yanaleta wivu, makelele, matukano, masingiziano


Kwa kumaliza, ninyi wote mukuwe na mawazo na nia moja, mupendane kama wandugu waamini, mukuwe wema na wanyenyekevu.


Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan