18 Nanyi vilevile mufurahi na kushiriki pamoja nami katika furaha yenu.
Basi ninawaomba musiregee kwa sababu ya mateso ninayopata kwa ajili yenu, kwa maana yanawaletea utukufu.
Hata nikitoa maisha yangu kuwa sadaka pamoja na imani yenu inayokuwa sadaka mbele ya Mungu, mimi ninafurahi na kushiriki pamoja nanyi wote.
Kama Bwana Yesu akitaka, ninangojea kisha muda kidogo kuwatumia Timoteo, kusudi nipate kutiwa moyo na habari nitakazopata kutoka kwenu.
Kwa kumaliza, wandugu zangu, mufurahi kwa ajili ya kuungana kwenu na Bwana. Hainiuzi kitu kuwaandikia tena maneno yale yale niliyowaandikia mbele. Hayo yote ni kwa ajili ya kuwakingia hatari.
Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!