Wandugu zangu, musikuwe kama watoto kwa kufikiri: lakini katika mambo mabaya, iwatokee kutenda kama watoto wachanga. Inafaa mafikiri yenu yakuwe kama ya watu wazima.
Ninyi munakuwa na kila kitu kwa uwingi: imani, usemi, ufahamu, kuwa na bidii ya kila namna na upendo munaokuwa nao kwetu. Kufuatana na hiyo mukuwe vilevile na uwingi katika kazi hii ya kuwa na moyo wa kutoa.
Kwa sababu hii hatuchoki kuwaombea ninyi, tangu siku tuliposikia habari zenu. Tunamwomba Mungu awawezeshe kujua kabisa mapenzi yake na kuwajaza hekima na akili inayotoka kwa Roho wake.
Kwa mwisho, wandugu, sisi tumewafundisha namna gani munavyopaswa kuishi kusudi mupate kumupendeza Mungu. Na kweli, ni vile munavyoishi. Na sasa, tunawaomba na kuwasihi kwa jina la Bwana Yesu, muendelee mbele vizuri zaidi katika mwenendo ule.
Wandugu, tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu. Inatufaa kufanya vile kwa maana imani yenu inaongezeka, nao upendo wenu ninyi kwa ninyi unazidi kuongezeka.